Karibuni kwenye Blogu Rasmi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Huu ni Uwanja wa Wananchi Kupata Taarifa Mbalimbali za Serikali na Masuala Mengine ya Kijamii, Kisiasa, na Kiuchumi. Blogu hii inaratibiwa na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali kupitia Idara ya Habari (MAELEZO).
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Adolf Nduguru, akifungua mafunzo ya Waratibu wa Biashara ya Huduma Ndogo za Fedha, jijini Dodoma, ambapo amewataka washiriki kuimarisha na kuhamasisha biashara ya huduma ndogo za fedha katika maeneo yao.
Na. Farida Ramadhani na Peter Haule, WFM, Dodoma
Serikali imeteua Waratibu wa kuhamasisha Biashara ya Huduma Ndogo za Fedha kwa lengo la kuimarisha usimamizi na uendelezaji wa Sekta Fedha nchini.
Hayo yalielezwa jijini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Adolf Ndunguru, wakati wa ufunguzi wa awamu ya kwanza ya mafunzo ya Waratibu wa Biashara ya Huduma Ndogo za Fedha.
Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi ya Serikali ya Mapinduzi Zanibar (SMZ) Bw. John Kilangi akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuhamasisha wananchi kurasimisha ardhi ili kuondoa migogoro na kuwawezesha kutumia hatimilki kujikwamua kiuchumi ikiwemo kuvutia uwekezaji.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama bilauli zilizotengenezwa na Bibi Ameniba Mberwa (kulia) wakati alipotembelea maonesho ya nne ya mifuko na programu za uwezeshaji wananchi katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha, leo Februari 9, 2021. Bibi Ameniba amewezeshwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii unaoratibiwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza mifuko na programu zote za uwezeshaji ifanyetathmini ya shughuli na huduma zake ili kubaini mafanikio, changamoto na maeneo yanayohitaji uboreshaji hususan eneo la masharti ya utoaji mikopo kwa wajasiriamali.
Pia, Waziri Mkuu ameitaka mifuko inayotoa dhamana kwa wafanyabiashara na wajasiriamali mbalimbali nchini, iimarishe usimamizi, uratibu na utendaji wake kwa kutengeneza mipango maalum ya kila mwaka inayoonesha malengo ya dhamana zitakazotolewa katika mwaka husika.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Innocent Bashungwa ameagiza Wasimamizi wa shule zote nchini kuhakikisha somo la Michezo linafundishwa shuleni.
Mhe. Bashungwa ameyasema hayo leo Februari 08, 2021 jijini Dodoma katika kikao kati yake, Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia ambacho kilijadili namna ya kuboresha Michezo katika shule za msingi na Sekondari.
“Sera ya Michezo ya mwaka 1995 ilikua imekosa Mpango Mkakati wa kuitekeleza vyema, na tayari rasimu ya mpango huo ipo, lengo la kikao hiki ni muendelezo wa utekelezaji wa vikao mbalimbali vya kuboresha sekta hii kwa kushirikiana na wizara hizi tatu” alisema Mhe. Bashungwa.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo ametoa agizo kwa Halmashauri zote nchini kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli za michezo, huku akiagiza Wakurugenzi katika halmashauri hizo kusimamia vyema miundombinu ya michezo na kuhakikisha maeneo ya michezo hayavamiwi.
“Nawaagiza walimu wakuu wa shule zote nchini, kusimamia vyema vipindi vya michezo kwa kuhakikisha vinafundishwa katika muda sahihi na wanafunzi wanashiriki vyema vipindi hivyo.
Na sisi upande wa Serikali tutasimamia vyema ajenda hiyo na tutahakikisha maafisa elimu Mkoa na Wilaya wanafuatilia michezo katika maeneo yao kwakua tunataka Tanzania iwe na wanamichezo wazuri wa kuisaidia nchi yetu” alisema Mhe. Jafo.
Naye Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amesema kuwa, Wizara yake itahakikisha inaandaaa na kuhuisha Mitaala iliyopo kuhusu somo la michezo ili somo hilo lilete tija kwa Taifa kwa kuzalisha wataalamu wengi wa fani hiyo.
“Kwakua tunafahamu Michezo ni ajira na inajenga afya, ni jukumu letu kuhakikisha tunaisimamia vyema na tayari katika shule za msingi kuna somo linaitwa Haiba na Michezo na katika shule za sekondari kuna somo linaitwa Elimu kwa njia ya Michezo (Physical Education), masomo hayo yanatengeneza wataalamu katika sekta hiyo” alisema Mhe. Joyce”.
Naye Naibu Waziri wa Wizara ya Habari Mhe. Abdallah Ulega ametoa wito kwa vyuo na shule zinazofundisha michezo kusimamia vyema ufundishaji wa masomo hayo kwakua ndio yanayosaidia kuzalisha wataalam wa kuendeleza michezo nchini.
Kikao hicho kimeazimia mambo mengi ikiwemo kutenga bajeti ya kutosha kwa ajili ya shughuli za michezo ya UMISETA na UMITASHUMTA.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa akieleza mipango mbalimbali ya kuendeleza michezo wakati wa kikao cha kujadili namna ya kuboresha michezo katika shule za msingi na sekondari, Kikao hicho kimekutanisha Wizara za Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo,Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia na Wizara ya TAMISEMI.
Na Shamimu Nyaki – WHUSM
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Selemani Jafo ametoa agizo kwa Halmashauri zote nchini kutenga maeneo kwa ajili ya shughuli za michezo, huku akiagiza Wakurugenzi katika halmashauri hizo kusimamia vyema miundombinu ya michezo na kuhakikisha maeneo ya michezo hayavamiwi.
Mhe. Jafo ameyasema hayo leo Februari 08, 2021 jijini Dodoma katika kikao kati ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Ofisi ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia kilichoandaliwa na Wizara ya Habari ambacho kilijadili namna ya kuboresha Michezo katika shule za msingi na Sekondari.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof Joyce Ndalichako akisisitiza jambo wakati wa kikao cha kujadili namna ya kuboresha michezo katika shule za msingi na sekondari, Kikao hicho kimekutanisha Wizara za Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo,Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia na Wizara ya TAMISEMI.
Katibu Mkuu Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Bw. Islam Seif Salum akieleza hatua zilizochukuliwa na zitakazochukuliwa na Wizara hiyo katika kuhakikisha kwamba urasimishaji biashara unaleta tija na kuzalisha ajira zaidi kama ilivyo dhamira ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
f Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Omar Othman Makungu (katikakati) akiongoza maandamano ya Maadhimisho ya Siku ya Sheria Zanzibar, wakiingia katika viwanja vya ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Jijijni Zanzibar, wakimalizia maandamano hayo yalioanzia katika viwanja vya Mahakama Kuu ya Zanzibar Vuga.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi amewaagiza Wenyeviti wa Mabaraza ya ardhi na Nyumba ya wilaya kutumia lugha ya Kiswahili katika kuandika hukumu.
Lukuvi alitoa maagizo hayo tarehe 5 Februari 2021 jijini Dodoma alipozungumza na Wenyeviti pamoja na Wasajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kwa nchi nzima kupitia Video (Video conference).
“Nasisitiza Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya mtumie lugha ya Kiswahili wakati wa kuandika hukumu zenu kama alivyoagiza Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli na nitashangaa kumuona mwenyekiti akiandika hukumu kwa lugha ya kiswahili’’ alisema Lukuvi
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (kushoto), Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA), Erasto Simon (katikati) na Mhandisi Mkuu wa Vituo vya Upokeaji wa Mafuta katika Bandari ya Dar es Salaam, Yona Malago ( kulia) wakikagua eneo la kupakulia mafuta bandarini wakati wa ziara ya waziri huyo ya kujiridhirisha kama kuna mafuta ya kutosha kukidhi mahitaji yanayohitajika nchini, iliyofanyika Februari 07, 2021.
Na Zuena Msuya – Dar es Salaam
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amewatoa hofu watanzania kwa kusema kuwa tishio la virusi vya ugonjwa wa corona halijaathiri upatikanaji wa mafuta nchini.
Aidha kuna ziada ya mafuta itakayotumika zaidi ya siku 30 na bado meli zinaendelea kupakua mafuta bandarini.
Afisa Mfawidhi, Kituo cha kutotolesha Vifaranga vya Samaki cha Ruhila, Emmanuel Maneno (wa kwanza kushoto) akimueleza jambo Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (katikati) alipotembelea Kituo hicho kilichopo Mkoani Ruvuma Februari 6, 2021. Wa kwanza Kulia ni Mkurugenzi, Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji WMUV), Dkt. Nazael Madalla.
Na Mbaraka Kambona, Ruvuma
Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah amesema kuwa Serikali imepanga kutumia shilingi milioni 110 kwa ajili ya kuimarisha miundo mbinu ya Kituo cha Kutotolesha Vifaranga vya Samaki cha Ruhila ili kiweze kuzalisha vifaranga vitakavyokidhi mahitaji yaliyopo sasa.
Dkt. Tamatamah aliyasema hayo alipotembelea kukagua shughuli zinazofanywa na kituo hicho kilichopo mkoani Ruvuma Februari 6, 2021.