Karibuni kwenye Blogu Rasmi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Huu ni Uwanja wa Wananchi Kupata Taarifa Mbalimbali za Serikali na Masuala Mengine ya Kijamii, Kisiasa, na Kiuchumi. Blogu hii inaratibiwa na Ofisi ya Msemaji Mkuu wa Serikali kupitia Idara ya Habari (MAELEZO).
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili kufungua majengo mapya na upanuzi wa huduma katika Kituo cha Afya cha Masumbwe Wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita akiongozana na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Dorothy Gwajima na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Selemani Jaffo leo Jjumatano Januari 27, 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika Kituo cha Afya cha Masumbwe wilayani Mbogwe leo Jjumatano Januari 27, 202
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Nane itakuja na ubunifu wa kutatua changamoto katika sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na kuhakikisha sekta hiyo inatengewa fedha za kutosha.
Ameyasema hayo leo katika Kikao na Wadau wa Elimu, Kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil, Kikwajuni Jijini Zanzibar, ukiwa na madhumuni ya kutafuta ufumbuzi juu ya matatizo yanayoikabili sekta ya elimu.
Rais Dk. Mwinyi alisema kwamba sekta ya elimu ni lazima ipewe kipaumbele maalum ili kuhakikisha malengo yake yaliyoyaweka yanafanyiwa kazi na kupatiwa ufumbuzi kwa kuwekewa fedha.
Bidhaa za vipodozi vyenye viambata sumu, vyakula na vinywaji ambavyo muda wake wa matumizi umepita (Expired produducts) zisizokidhi ubora wa viwango yenye thamani ya shilingi milioni 40 ambazo ziliondolewa sokoni na Wakaguzi wa TBS kanda ya kati na kuteketezwa katika dampo la Chidachi Dodoma, Leo Januari 27,2021 (Picha na Eliud Rwechungura)
Na Eliud Rwechungura
Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limeteketeza bidhaa zisizokidhi ubora wa viwango zenye thamani ya shilingi milioni 40 ambazo ziliondolewa sokoni na Wakaguzi wa TBS kanda ya kati kuanzia mwezi Novemba, 2020 hadi Januari 15, 2021.
Zoezi hilo la uteketezaji bidhaa hizo limefanyika katika dampo Chidachi – Dodoma, leo Januari 27, 2021
Bidhaa zilizoharibiwa ni pamoja na vipodozi vyenye viambata sumu, vyakula na vinywaji ambavyo muda wake wa matumizi umepita (Expired produducts) vilivyopatikana katika maduka mbalimbali yaliyopo katika Mikoa ya Dodoma, Tabora na Singida.
Sheria ya Viwango Na. 2 ya mwaka 2009 pamoja na Sheria ya Fedha Na.8 ya mwaka 2019 mbali na majukumu mengine zimelipa mamlaka Shirika kuondoa bidhaa hafifu sokoni na kuziharibu ama kuzirudisha zinakotoka pindi zinapobainika kuwa hazifai kwa matumizi ya binadamu.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Abdallah Ulega akigawa zawadi ya mipira kwa uongozi wa Shule ya Sekondari Dodoma kwa ajili ya shughuli za michezo shuleni hapo, wakati alipofanya ziara ya kukagua shughuli shughuli hizo leo Januari 27, 2021 Jijini Dodoma. Wanaoshuhudia ni Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Antony Mavunde, uongozi wa Jiji hilo pamoja na wanafunzi wa shule hiyo.,
Na Shamimu Nyaki – WHUSM, Dodoma
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Ulega ameagiza viongozi na wasimamizi wa shule zote nchini kusimamia vyema vipindi vya michezo shuleni.
Mhe. Ulega ameyasema hayo leo Januari 27, 2021 katika ziara yake ya kukagua shughuli za michezo shuleni, ambapo alitembelea Shule ya Sekondari Dodoma pamoja na Shule ya ya Michezo ya Fountain Gate.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi amepiga marufuku Halmashauri, Taasisi na watu binafsi kuchukua maeneo ya wananchi bila kulipa fidia.
Akizungumza hivi karibuni mkoani Singida wakati wa ziara yake ya kikazi katika mkoa huo, Lukuvi alisema kumekuwa na tabia ya baadhi ya Halmashauri na Taasisi kuchukua maeneo ya wananchi bila ya kuwalipa fidia kwa maelezo maeneo hayo kuhitajika kwa ajili ya shughuli za kimaendeleo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Butengo Chato mkoani Geita kabla ya kuzindua Shamba kubwa la Miti lenye jumla ya hekari elfu 69 mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akipanda mti wakati akizundua rasmi Shamba la Miti lililopewa jina la Silayo wilayani Chato mkoani Geita leo Jumatano Januari 27, 2021. Shamba hilo, ambalo ni miongoni mwa mashamba 23 ya Serikali yanayosimamiwa na kuendelezwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimwagilia maji mti alioupanda kama kumbukumbu mara baada ya kuzindua shamba la Miti lenye hekari elfu 69 katika eneo la Butengo Chato mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akipanda juu na kusalimiana na mafundi wanaojenga mtambo wa kutibia maji unaondelea kujengwa kwenye kilima kilichopo katika Kijiji cha kituntu, kata ya Kyaka ambapo mradi wa maji Kyaka Bunazi unajengwa.
Na Allawi Kaboyo – Missenyi.
Waziri wa maji, Jumaa Aweso amemtaka Mkandarasi anayetekeleza mradi wa maji Kyaka Bunazi kufanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa muda ambao umepangwa kwa mujibu wa mkataba na kusisitiza kuwa hakutokuwa na muda wa nyongeza kwenye mradi huo.
Mhe. Aweso ametoa maagizo hayo Januari 26, mwaka huu alipotembelea mradi huo ili kujionea maendeleo yake akiwa ameambatana na Naibu Katibu Mkuu, Mhandisi Nadhifa Kemikimba, ambapo mradi huo unajengwa na Mkandarasi aitwaye China Civil Engineering Consultant & Cooperation na kusimamiwa na Mamlaka ya Maji Mwanza kwa gharama ya shilingi bilioni 15.1 hadi kukamilika kwake.
Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) umeongeza mapato yake ya ndani (Own Sources) kutoka Shilingi Bilioni 4 kwa mwaka wa fedha 2006/07 hadi kufikia Shilingi Bilioni 54 kwa mwaka wa fedha 2019/20.
Hayo yameelezwa na Mtendaji Mkuu wa TEMESA, Mhandisi Japhet Maselle, wakati akiwasilisha taarifa kuhusu muundo na majukumu ya Wakala huo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu jijini Dodoma.
Mhandisi Maselle, amesema kuwa ongezeko hilo limeifanya TEMESA Kupunguza utegemezi wake kwa Serikali katika kujiendesha kwake na kuweza kuchangia Mfuko Mkuu wa Serikali kila mwaka.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile akizungumza na Watendaji Wakuu wa Makampuni ya simu nchiniwengine kutoka kulia ni katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma, wengine kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula, Naibu wake dkt Jim Yonazi na Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano Clarence Ichwekeleza.
Na Faraja Mpina- WMTH
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Serikali kupitia Wizara yake inashirikiana na wadau wa sekta ya mawasiliano kuhakikisha inatatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo ili wananchi waweze kupata huduma bora za mawasiliano kwa gharama nafuu katika maeneo yote nchini.
Amezungumza hayo katika kikao chake cha majadiliano na Watendaji Wakuu wa makampuni ya simu Tanzania kilichofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma kwa lengo la kutatua changamoto na kuwa na mkakati wa pamoja wa kuongeza wigo wa mawasiliano ya kasi ya simu na data nchini.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya – Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Dkt. John Jingu akizungumza na wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Tanzania Bara katika kikao kazi kilichokutanisha wadau wa hao na Serikali kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar Es Salaam
Na Mwandishi wetu,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imekutana na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali katika kikao kazi cha kuweka mwelekeo wa Ushirikiano miongoni mwao na kutafuta ufumbuzi wa changamoto katika kufikia maendeleo yanayokusudiwa.
Kikao hicho cha kihisitoria, kimefanyika Jijini Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi katika ufunguzi wa kikao hicho alikuwa Katibu Mkuu, Wizara ya Afya – Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Dkt. John Jingu na kuhudhuriwa na washiriki zaidi ya 350 kutoka Serikalini na Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.