Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

TEWW Itekeleze Majukumu Yaliyokusudiwa
Aug 20, 2020
Na Msemaji Mkuu

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako akipewa maelezo na Mkuu wa Idara ya Shule Huria na Elimu kwa Umma juu ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima alipotembelea Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam 19.08.2020.  Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Dkt. Naomi Katunzi (picha na TEWW)

  Na Mwandishi Wetu- TEWW 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Joyce Ndalichako ameitaka Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) kuhakikisha inatelekeza ipasavyo Mradi wa Kuinua Ubora wa Elimu ya Sekondari (SEQUIP) kwa kuwa TEWW moja ya Taasisi inayotekeleza mradi huo.

Waziri Ndalichako ametoa maagizo hayo jijini Dar es Salaam alipokutana na kufanya mazungumzo na Wajumbe wa Baraza la Usimamizi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima.

Amesema ni vizuri mradi huo ukatekelezwa ipasavyo ili malengo ya mradi yaweze kufikiwa ambapo moja kati ya malengo hayo ni kuwezesha mtoto wa kitanzania kuendelea kupata elimu bora.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako (katikati), Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi TEWW Dkt. Naomi Katunzi (Kulia kwake), Mkurugenzi wa TEWW Dkt. Michael Ng’umbi (kushoto kwake) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Usimamizi la TEWW pamoja na Menejimenti ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima baada ya kumaliza ziara ya kutembelea taasisi hiyo jana 19.08.2020 jijini Dar es Salaam.
 

Aidha, Prof. Ndalichako amesisitiza TEWW kuendelea kufanya kazi ninazoendana na dhima wa uanzishwaji wa Taasisi hiyo ikiwepo utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa ya Kisomo maarufu kama ‘NALMES’ pamoja na kuandika maandiko kwa ajili ya miradi mingine kwa ajili ya kuwawezesha watanzania. 

Katika hatua nyingine, Waziri Ndalichako amepongeza Baraza la Usimamizi wa TEWW kwa kufanya majukumu yake kwa ufanisi mkubwa toka ilivyozinduliwa mnamo Agosti, 2018.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Dkt. Michael Ng’umbi amemwakikishia Waziri kuwa TEWW itatekeleza mkakati wa Kisomo wa Kitaifa (NALMES) na ule wa SEQUIP kama ambavyo ilivyokusudiwa kwa ajili ya maslahi mapana ya Tanzania.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi