Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mhe. Waziri Makonda Akagua Miradi ya Maendeleo Arusha
Feb 04, 2026
Mhe. Waziri Makonda Akagua Miradi ya Maendeleo Arusha
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Arusha mjini, Mhe. Paul Makonda akikagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika jiji la Arusha.
Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Arusha mjini, Mhe. Paul Makonda amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika jiji la Arusha ikiwa ni utekelezaji wa ahadi za serikali na kuimarisha miundombinu katika kipindi hiki ambacho Arusha itakuwa katika Mashindano ya AFCON 2027.

Mhe. Makonda amefanya ziara hiyo tarehe 3 Februari, 2026 ambapo alikagua miradi ya miundombinu, huduma za kijamii na maendeleo iliyopo maeneo ya Arusha mijini.

Makonda pia alijikita kwenye ukaguzi wa sekta mbalimbali za miundombinu ikiwemo ujenzi wa Stendi ya mabasi ya mkoa wa Arusha, ujenzi wa Soko la Kilombero na ujenzi wa jengo jipya la Halmashauri ya jiji la Arusha

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi