Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Feb 13, 2019
Na Msemaji Mkuu

Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), TAHA- Taasisi inayosimamia Wadau wa Mbogamboga na Matunda kwa kushirikiana na Shirika la Biashara la Kimataifa (ITC) inatekeleza mradi wenye lengo la kuboresha masoko ili kuongeza mauzo ya Nje (MARKUP).

Hivyo, tunapenda kuwaataarifu wadau wa zao la parachichi nchini kushiriki katika mradi huo ili kufaidika na fursa ya upatikanaji wa mitaji ya biashara, mafunzo ya  namna ya kufikia soko la nje,kuwa sehemu ya ushiriki wa Maonesho mbalimbali yatakayoenda sambamba na  Mikutano ya kibiashara (B2B). KAMPUNI ZITAKAZOFAIDIKA NI ZILE TU ZITAKAZOKIDHI VIGEZO.

Ili kujisajili tafadhali tembelea tovuti www.tantrade.go.tz ili kujaza dodoso.Kwa taarifa zaidi piga simu Na. 0787 654386.

Mwisho wa kutuma maombi ni tarehe 14 Februari, 2019.

Imetolewa:

Theresa H. Chilambo

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano

12 Februari, 2019

 

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi