Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Majaliwa Atembelea Maonesho ya Nne ya Mifuko na Programu za Uwezeshaji Wananchi Arusha
Feb 09, 2021
Na Msemaji Mkuu

Waziri Mkuu amesema sambamba na programu na mifuko hiyo, Halmashauri 185 Tanzania Bara zimefanikiwa kutoa shillingi bilioni 93.3 kupitia mifuko ya uwezeshaji wa makundi maalum ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Fedha hizo, zimewezesha upatikanji wa mikopo yenye masharti nafuu kwa vikundi 32,553.  

“Nitumie nafasi hii kuendelea kusisitiza kwamba kila Halmashauri ihakikishe inatenga asilimia 10 ya mapato yake ya fedha za ndani ili zitumike kutoa mikopo kwa vijana (asilimia 4), wanawake (asilimia 4) na watu wenye ulemavu (asilimia 2). Pia, natoa wito kwa Mabaraza ya Madiwani katika kila Halmashauri kufuatilia utekelezaji wa maagizo haya ya Serikali ambayo yameridhiwa na Bunge na kutungiwa sheria mahsusi.”

Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Beng’i Issa amesema baraza hilo linajukumu la kusimamia, kufuatilia na kuratibu shughuli mbalimbali za uwezeshaji wananchi kiuchumi ikiwemo mifuko na programu za uwezeshaji.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi