Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

JKT Yatakiwa Kukamilisha Ujenzi Ikulu kwa Wakati
Aug 22, 2020
Na Msemaji Mkuu

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi akitoa neno la shukrani kwa Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu kwa kutembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Ikulu Chamwino jijini Dodoma.

Na Mwandishi Wetu- Dodoma

Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Balozi John Kijazi amemtaka  mkandarasi wa Ikulu ya Chamwino  mkoani Dodoma kuhakikisha anakamilisha mradi wa ujenzi kama ilivyopangwa.

Ametoa wito huo  wakati wa ziara ya makatibu wakuu na manaibu Katibu Wakuu  katika eneo la ujenzi wa mradi huo leo Agosti 21, 2020.

“Kazi ya ujenzi inaendelea vizuri na kasi inaridhisha hivyo ongezeni kasi zaidi ili mradi ukamilike ikiwezekana kabla ya muda uliopangwa bila kuathiri ubora wa majengo,” alisisitiza Balozi Kijazi

Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali  Rajab Mabele akizungumza wakati Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu kutoka Wizara mbalimbali wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi, John Kijazi walipotembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Ikulu Chamwino jijini Dodoma.

Akifafanua, Balozi Kijazi amesema, Serikali imewapa JKT kazi ya ujenzi huo kwa sababu inawaamini na inaamini watatekeleleza kwa gharama nafuu ikilinganishwa na wakandarasi wengine.

Aliongeza kuwa uamuzi wa kuwapa kazi ya ujenzi wa Ikulu ni wa kimkakati na una manufaa kwa Taifa.

Makatibu Wakuu kutoka Wizara mbalimbali wakiweka zege kwenye jiwe la msingi la ujenzi wa Ikulu Chamwino baada ya kutembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Ikulu hiyo jijini Dodoma.

Aidha, aliipongeza JKT kwa kazi nzuri mnayofanya katika kutekeleza mradi huo  na kuwataka  kila kazi ambayo mkandarasi anafanya ilenge kukamilisha kazi ya ujenzi kwa wakati uliopangwa.

Naye Mkurugezi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Rajab Mabele amesema kuwa ujenzi wa Ikulu unaendelea kwa kasi kutokana na ushirikiano mzuri uliopo  kati ya JKT na TBA ambao ni wasimamizi wa mradi huo.

Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu kutoka Wizara mbalimbali wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Balozi John Kijazi wakiendelea na ziara.

“Tunamshukuru Mhe Rais na Amiri Jeshi Mkuu, Dkt John Pombe Magufuli kwa kuendelea kutuamini na kutupa kazi  hii ya ujenzi wa Ikulu hapa Chamwino,”. 

Akifafanua amesema kuwa miradi iliyotolewa na wizara mbalimbali imeiwezesha SUMA JKT kununua mitambo, vifaa vya kisasa, magari na hivyo kuongeza ufanisi katika utendaji.

Ujenzi wa Ikulu Chamwino ukiendelea kwa kasi na unatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba, 2020.

Aliongeza kuwa  SUMA JKT itaendelea kufanya kazi usiku na mchana kukamilisha mradi huu kwa wakatiambapo ,katika kutunza mazingira wamepanda miti zaidi ya 5600 katika eneo hilo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi