Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Waziri Mkuu Amwakilisha Rais Magufuli Mkutano wa TICAD
Aug 29, 2019
Na Msemaji Mkuu

*Asema nchi inahitaji teknolojia ya uhakika kufanikisha uchumi wa viwanda

[caption id="attachment_46354" align="aligncenter" width="750"] Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Rais waTogo, Faure Gnassingbe (kulia) wakipiga makofi katika ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on Africa Development (TCAD7) uliofunguliwa na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe kwenye Ukumbi wa hoteli ya Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019.[/caption]

Na: Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema Tanzania inahitaji kuwa na tekinolojia mpya na ya uhakika ili kufanikisha mkakati wa Seikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli wa kukuza uchumi na kufikia wa kati ifikapo 2015 kupitia sekta ya viwanda.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Agosti 28, 2019) katika Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on African Development (TCAD 7) uliofunguliwa na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe kwenye ukumbi wa hoteli ya Pacifico Yokohama nchini Japan.

[caption id="attachment_46355" align="aligncenter" width="750"] Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi (kushoto) wakisikiliza hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on Africa Development (TCAD7) uliofunguliwa na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe kwenye Ukumbi wa hoteli ya Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019. [/caption]

Waziri Mkuu ambaye amemwakilisha Rais Dkt. John Magufuli katika mkutano huo amesema kwamba ujenzi na uendeshaji wa uchumi wa viwanda   unahitaji sana teknolojia kutoka  ndani na nje ya nchi.

Amesema ujezi  wa uchumi wa viwanda utajikita katika matumizi ya malighafi yanayopatikana nchini kama vile mazao ya kilimo, uvuvi, mifugo na madini kwani Tanzania imebarikiwa kuwa na ardhi nzuri na hali ya hewa  inayofaa kwa kilimo pamoja na kuwa mali asili nyingi.

[caption id="attachment_46356" align="aligncenter" width="750"] Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na viongozi Wakuu wa Nchi za Afrika wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on Africa Development (TCAD7) uliofunguliwa na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe kwenye Ukumbi wa hoteli ya Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019. [/caption] [caption id="attachment_46357" align="aligncenter" width="750"] Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi waku wa Nchi za Afrika na Japan katika ufunguzi wa Mkutano wa Saba wa Tokyo International Conference on Africa Development (TCAD 7) uliofanyika kwenye Ukumbi wa hoteli ya Pacifico Yokohama nchini Japan, Agosti 28, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)[/caption]

Waziri Mkuu amesema hivi sasa Tanzania inaandaa miundombinu na huduma mbalimbali zitakazofanya uwekezaji katika sekta ya viwanda ufanyike katika mazingira yanayokidhi matarajio ya wawekezaji na wateja wao.

Ametoa mifano wa  ujenzi wa bwawa la kufua umeme la Nyerere katika mto Rufiji, ujenzi wa Reli ya kisasa ya SGR , ujenzi wa barabara za lami, ufufuaji wa Shirika la Ndege la Tanzania na upanuzi wa Bandari za Dar es salaam, Mtwara na Tanga kuwa ni baadhi ya mipango ya Serikali ya kuifanya nchi iwe na sifa na viwango  katika suala la uwekezaji wa  viwanda.

“Utaratibu wa Blue Print ulioandaliwa na Serikali kwa lengo la  kuondoa kero mbalimbali katika uwekezaji na biashara nchini Tanzania ni mfano hai unaodhihirisha kamba Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kushirikiana na sekta binafsi kujenga uchumi wa viwanda.”

Awali,akifungua mkutano huo, Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe amesema katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita,  uwekezaja uliofanywa  Barani Afrika na wawekezaji binafsi kutoka nchini Japan umefikia Dola za Marekani bilioni 20. Ameahidi kuwa uwekezaji huo utaendelea kuengezeka.

Viongozi mbali mbali kutoa nchi za Afrika wamehudhuria mkutano huo akiwemo Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Rais wa Rwanda, Paul Kagame, Rais Uganda, Yoweri Musseveni pamoja na Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravini Kumar.

Waziri Mkuu ameambatana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi  na viongozi mbalimbali kutoka Serikali ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

       

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi