Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Waziri Dkt. Mabula Ashiriki Mkutano wa Majiji Kisumu Kenya
May 22, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Kisumu, KENYA

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dkt. Angeline Mabula ameshiriki mkutano wa tisa wa viongozi wa Majiji huko Kusumu nchini Kenya.

Mkutano huo uliomalizika Mei 222, 2022 uliwakutanisha maelfu ya wadau ulijadili maendeleo ya miji Barani Afrika na ulifunguliwa kwenye mji wa Kisumu, Magharibi mwa Kenya.

Mbali na maelfu ya Wadau, Watalaam na Viongozi wa Miji waliokutana kwenye mkutano huo, viongozi kadhaa wa mataifa ya Afrika, pamoja na wale waliostaafu nao walihudhuria mkutano huo.

Aidha, kupitia mkutano huo Waziri, Dkt. Angeline Mabula alikabidhiwa Tuzo ya Heshima (Commitment in Fevour of the African Movement of the Territorial Government) kwa niaba ya Rais Mstaafu Jakaya Kikwete iliyotolewa na Taasisi ya United Cities and Local Government of Africa (UCLG Africa).

Miongoni mwa mambo yaliyojadiliwa kwenye mkutano huo wa kimataifa maarufu kwa jina la "Africities ni kuhusu hali ya miundombinu kwenye miji mbalimbali na namna bora ya kuimarisha maisha ya wakazi wa miji hiyo.

Mameya wa Miji mbalimbali, Mawaziri wa Serikali za Mitaa walihudhuria mkutano huo na kutafuta suluhu ya changamoto zinazowasumbua wakazi wa miji yao kama vile mipangilio mibaya ya majengo, mitaa pamoja na changamoto za  upatikanaji wa umeme.

Huo ni mkutano wa kwanza kufanyika katika jiji ambalo lina wakazi kati ya 50,000 na Laki tano ambapo kwa mujibu wa Sensa ya mwaka 2009 lina watu 409,000.

Kauli mbiu ya mkutano huo ni mchango wa miji inavyoweza kuchangia utekelezwaji wa dira ya Umoja wa Mataifa ya mwaka 2030 na Umoja wa Afrika mwaka 2063.

Majiji mengine ambao yamewahi kuandaa mkutano huu unaofanyika kila baada ya miaka mitatu tangu1998 jijini Abidjan, umewahi pia kufanyika jijini Johannersburg, Dakar Kule Senegal na Marakesh nchini Morocco.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi