Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Wananchi 62 Wafanyiwa Vipimo vya Kuangalia Moyo Unavyofanya Kazi JKCI
Mar 29, 2019
Na Msemaji Mkuu

Na Mwandishi Maalum – JKCI

 Jumla ya watu 62 wamefanywa vipimo vya kuangalia jinsi moyo unavyofanya kazi (Echo Cardiogram)  na umeme wa moyo (ECG) wakati wa punguzo la gharama za matibabu kwa wagonjwa wa kulipia lililotolewa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).

Punguzo hilo lilitolewa hivi karibuni na Taasisi hiyo ikiwa ni sehemu ya  kusherehekea ushindi wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu  kwa kuifunga timu ya Uganda mabao 3-0 na  kuweza kushiriki katika mashindano ya  Taifa Bingwa Barani Afrika AFCON. 2019.

Akiongea na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Tiba Shirikishi ambaye pia ni daktari bingwa wa magonjwa ya moyo  Dkt. Delila Kimambo alisema  kati ya wagonjwa 62 waliopima afya zao nane walikuwa ni watoto.

Dkt. Delila alisema katika kusherehekea ushindi wa timu ya Taifa Taasisi hiyo imeona  ni vyema kufungua milango  na kuwahamasisha wananchi kujitokeza kupima afya ya moyo.

“Kati ya watu 62 tuliowapima  19 tuliwakuta na matatizo ya moyo ambapo wa nne wanatakiwa kufanyiwa  uchunguzi wa mishipa ya damu ya moyo, mmoja kati yao ameshafanyiwa na kukutwa na tatizo la kuziba kwa mishipa miwili ya damu ameshazibuliwa mshipa mmoja na anaendelea vizuri”,.

“Wengine  wanne walikutwa na tatizo la valvu ambapo  wawili wanatakiwa kufanyiwa  upasuaji wa kubadilisha valve. Wengine tumewakuta na  shinikizo la juu la  damu”,.

 “Zoezi hili limefanyika vizuri, tunafahamu kuwa kuna wananchi ambao huwa wanahitaji vipimo vya moyo kwa dharula na hawawezi kufika kwetu kutokana na shida mbalimbali za maisha, hivyo tulitoa punguzo hili la bei  ili kuwafungulia milango ya kupata matibabu ya vipimo vinavyoweza kugundua kama mtu ana magonjwa ya moyo”, alisema Dkt. Delila.

Dkt. Delila alimalizia kwa kuwaomba  watanzania kuwa na utamaduni wa kupenda kupima afya zao mara kwa mara ,kupata matibabu na majibu ya magonjwa yanayowasumbua  kutoka  kwa wataalamu wa magonjwa husika.

Kwa upande wake Frank Karia ambaye ni makazi wa Mwanza alisema alipewa Rufaa  kutoka hospitali ya rufaa ya Bugando na kufika JKCI siku ya Jumatatu ambapo kulikuwa na punguzo la bei na kubahatika kufanyiwa vipimo vya  ECHO na ECG baada ya kufanyiwa vipimo aligundulika kuziba kwa mishipa  miwili inayopeleka damu kwenye moyo.

“Baada ya kukutwa na tatizo ndani ya wiki moja tayari nimeshazibuliwa mshipa mmoja wa damu na hali yangu inaendelea vizuri kama unavyoniona, baada ya wiki mbili nitarudi kliniki . Leo tarehe 29/03/2019nimeruhusiwa kwenda nyumbani, kwa kweli sikutegemea kama ningepata huduma hii kwa kipindi cha wiki moja” alisema  Karia.

Alisema huduma zinazotolewa na Taasisi hiyo ni  za kimataifa na kuwaomba waendelee kutoa elimu kwa umma ili wananchi wafahamu zaidi huduma zinazotolewa.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi