Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Wakulima na Wasindikaji wa Alizeti Watakiwa Kutumia Tafiti Kuongeza Tija
Dec 19, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_39093" align="aligncenter" width="900"] Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara kutoka Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Bw. Wilson Malosha akisisitiza jambo wakati akifungua warsha ya siku moja kwa wadau wa sekta ndogo ya uzalishaji na usindikaji wa alizeti hapa nchini iliyoandaliwa na Taasisi ya sekta binafsi (TPSF) leo Jijini Dodoma na kushirikisha wadau mbalimbali kutoka katika taasisi na mikoa mbalimbali. Warsha hiyo ililenga kujadili mafanikio yaliyopatikana baada ya Serikali kuongeza ushuru wa forodha wa asilimia 25 kwenye mafuta ghafi ya kula yanayoagizwa kutoka nje ya nchi.[/caption]

Na; Mwandishi Wetu

Wakulima na Wasindikaji wa mafuta ya alizeti wametakiwa kutumia taarifa za tafiti mbalimbali kusaidia katika kukuza sekta hiyo ambayo ina mchango mkubwa katika ujenzi wa uchumi wa viwanda.

Akizungumza wakati akifungua warsha ya siku moja iliyoandaliwa na Taasisi ya sekta binafsi Tanzania (TPSF) Jijini Dodoma kwa wasindikaji na wawakilishi wa wakulima  wa zao hilo, Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Biashara kutoka  Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji Bw. Wilson Malosha amesema kuwa ni vyema wazalishaji hao na wakulima wakatumia tafiti mbalimbali zilizofanyika  kuongeza tija .

[caption id="attachment_39094" align="aligncenter" width="897"] Makamu Mwenyekiti wa Chama cha wasindikaji wa alizeti (TASUPA) B w. Enock Ndondolo akizungumzia umuhimu wa sekta hiyo katika kutatua changamoto ya kukuza soko la mafuta yanayozalishwa hapa nchini kutokana na alizeti.semina hiyo imeandaliwa na Taasisi ya Sekta binafsi (TPSF). Warsha hiyo ililenga kujadili mafanikio yaliyopatikana baada ya Serikali kuongeza ushuru wa forodha wa asilimia 25 kwenye mafuta ghafi ya kula yanayoagizwa kutoka nje ya nchi.[/caption] [caption id="attachment_39095" align="aligncenter" width="900"] Mwenyekiti wa Chama cha wasindikaji wa alizeti (TASUPA) Bw. Ringo Iringo akizungumzia umuhimu wa kukuza uzalishaji na kutatua changamoto zilizopo katika sekta ndogo ya uzalishaji mafuta kupitia zao la alizeti. Warsha hiyo ililenga kujadili mafanikio yaliyopatikana baada ya Serikali kuongeza ushuru wa forodha wa asilimia 25 kwenye mafuta ghafi ya kula yanayoagizwa kutoka nje ya nchi.[/caption]

Warsha hiyo ililenga kujadili mafanikio yaliyopatikana baada ya Serikali kuongeza ushuru wa forodha wa asilimia 25 kwenye mafuta ghafi ya kula yanayoagizwa kutoka nje ya nchi.

‘’ Kila mmoja katika eneo lake ana jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa anachangia katika kuiwezesha nchi yetu kupunguza au kuondoa utegemezi wa mafuta ya kula kutoka nchi za nje kwa kuongeza uzalishaji wenye tija kwa kutumia alizeti tunayozalisha”.Alisisitiza Malosha

Akifafanua amesema kuwa mikakati ya pamoja inahitajika kati ya wazalishaji na Serikali ili kuwezesha azma yakukuza uzalishaji  wa mafuta na alizeti kukua kwa kasi inayoendana na mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi ili kuchangia katika kukuza uchumi.

[caption id="attachment_39096" align="aligncenter" width="900"] Mratibu wa Taasisi ya Best Dialogue Bi. Manka Kway akizungumza wakati wa warsha ya siku moja kwa wadau wa sekta ya alizeti wakiwemo wasindikaji na wawakilishi wa wakulima wa zao hilo.[/caption] [caption id="attachment_39097" align="aligncenter" width="900"] Sehemu ya washiriki wa warsha hiyo ya siku moja kwa wadau wa sekta ya alizeti wakiwemo wakulima na wazalishaji wa mafuta ya zao hilo.[/caption]

Aliongeza kuwa Taifa letu limejaliwa ardhi yenye rutuba kwa ajili ya uzalishaji wa zao hilo na kutaja baadhi ya mikoa hiyo kuwa ni Morogoro na Singida.

Kuongeza uzalishaji katika sekta hiyo kutachochea maendeleo ya viwanda na kupunguza fedha za kigeni zinazotumika katika kuagiza mafuta nje ya nchi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Chama cha  wasindikaji wa alizeti  Bw. Ringo Iringo amesema kuwa warsha hiyo itasaidia kuja na mikakati ya pamoja na kila mdau ataona eneo analopaswa kuchukua hatua  katika kuhakikisha kuwa sekta hiyo inakua na kuchangia katika kukuza uchumi.

[caption id="attachment_39099" align="aligncenter" width="808"] Mkurugenzi Mtendaji wa Ukanda Maalum wa uendelezaji Kilimo wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT) Bw. Geoffrey Kurenga akizungumza wakati wa semina hiyo. (Picha zote na MAELEZO)[/caption]

Aliongeza kuwa vikosi kazi vilivyoundwa kupitia Baraza la Biashara la Taifa vitatoa mchango mkubwa katika kutoa mapendekezo ya namna bora ya kutatua changamoto zilizopo ili kukuza sekta hiyo.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bw.  amesema kuwa Semina hiyo imewashirikisha viongozi wa vyama vya wazalishaji na wasindikaji wa alizeti wa mikoa takribani 19.

Warsha  hiyo imeshirikisha Ofisi ya Waziri Mkuu, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), wawakilishi wa wakulima wa alizeti na wasindikaji wa alizeti kutoka katika mikoa takribani 19 ya hapa nchini.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi