Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Wabunge Kuingia Darasani Somo la Maadili
Jun 30, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_4895" align="aligncenter" width="750"] Afisa Uhusiano wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu JK Nyerere Bi Evelyn Mpasha (kushoto) akifurahia Jambo na baadhi ya wananchi waliotembelea banda la Chuo hicho katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julias.K Nyerere,barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam.[/caption]

Na: Lilian Lundo

Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kinatarajia kufundisha programu ya uongozi maadili na utawala bora kwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo watasoma kwa awamu, mara baada ya kumalizika kwa Bunge la Bajeti.

Hayo yamesemwa na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Chuo hicho, Evelyne Mpasha leo jijini Dar es Salaam katika maonesho ya saba saba  ya 41 yanayoendelea Jijini humo.

Alisema Chuo hicho kimejizatiti kurejesha maadili kwa viongozi na Watanzania kupitia programu ya uongozi ya maadili na utawala bora inayotolewa chuoni hapo.

  [caption id="attachment_4897" align="aligncenter" width="750"] Mhadhiri wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Julias Nyerere Bw. Tiberius Mlowosa akiwaonesha baadhi ya wananchi Jarida la Chuo hicho walipotembelea banda hilo katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu J.K Nyerere,barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam. (Picha na Frank Mvungi)[/caption]

Mpasha amesema, Chuo hicho kilianzishwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1961 kikiwa na lengo la kufundisha viongozi wa Serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) maadili na uzalendo kwa nchi.

"Tangu kuanza mfumo wa vyama vingi nchini, Chuo kimekuwa kikijihusisha na utoaji wa programu za kitaaluma na  kuanzia mwaka 2015 chuo kimerejesha tena kozi ya uongozi na maadili," amesema Mpasha.

Amesema kuwa, kozi hiyo hutolewa kwa viongozi walio katika ngazi ya maamuzi kutoka Taasisi za Umma na Binafsi ambapo  hufundishwa masuala ya uzalendo, utaifa na maendeleo ya nchi.

Aidha, amesema Chuo kimepokea viongozi mbalimbali kutoka katika Halmashauri mbalimbali, Taasisi za Serikali na zisizo za Kiserikali kwa ajili ya kujifunza programu hiyo.

Nae, Mhadhiri wa Chuo hicho, Tiberius Mlowosa amesema kumekuwepo na  viongozi wengi wanao hujumu uchumi wa nchi kutokana na kukosa mafunzo ya uongozi na maadili.

"Kama viongozi wote walio ngazi ya maamuzi wangepata mafunzo ya uongozi maadili na utawala bora, tusingekuwa na masuala ya EPA wala ESCROW," amesema Mlowosa.

 Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere kinatoa programu nyingine nje ya programu hiyo ya uongozi ambazo ni Utawala na Rasilimali Watu, Usimamizi wa Biashara, Maendeleo ya Jamii, Uhasibu, Ununuzi na Ugavi kuanzia ngazi ya cheti .

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi