Viongozi Wakiwasili Arusha Kushiriki Kumbukizi ya Sokoine
Apr 11, 2024
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda wakati alipowasili mkoani Arusha kwa ajili ya kushiriki Ibada Maalum ya kumbukizi ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine itakayofanyika kesho tarehe 12 Aprili, 2024 Monduli.
Na
Mwandishi Wetu
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kisongo jijini Arusha Aprili 11, 2024. Kesho atashiriki katika Ibada Maalum ya Kumbukumbu ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine itakayofanyika Moduli. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM, Mkoa wa Arusha Loy Thomas Ole Sabaya.Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda alipowasili kwenye uwanja wa Ndege wa Kisongo jijini Arusha Aprili 11, 2024. Kesho atashiriki katika Ibada Maalum ya Kumbukumbu ya miaka 40 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Edward Moringe Sokoine itayofanyika Monduli Juu. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Loy Thomas Ole Sabaya.