Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Uteuzi
Aug 12, 2017
Na Msemaji Mkuu

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ikulu, Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Bernard Hezron Konga kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Bw. Bernard Hezron Konga umeanza tarehe 09 Agosti, 2017.

Kabla ya uteuzi huo Bw. Bernard Hezron Konga alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam

12 Agosti, 2017

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi