Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Utekekezaji Mradi wa HEET Nelson Mandela Wafikia Asilimia 30
Feb 27, 2024
Utekekezaji Mradi wa HEET Nelson Mandela Wafikia Asilimia 30
Naibu Makamu Mkuu wa Taasisi na Mratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela, Prof. Suzana Augustino akiongea wakati wa kikao cha kikanuni cha waratibu wa mradi wa Taasisi zinazotekeleza mradi huo Februari 27, 2024 jijini Dar es Salaaam.
Na Mwandishi Wetu

Waratibu wa Mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi kwa Elimu ya Juu (HEET) kutoka Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson wameshiriki kikao cha Kikanuni kwa lengo la kujadili utekelezaji wa mradi.

Mkurugenzi Elimu ya juu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msoffe akiongea na wajumbe wa kikao cha  Kikanuni  kilichoshirikisha Taasisi za Elimu ya Juu zinazotekeleza mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi kwa Elimu ya Juu  (HEET ) Februari 27,2024 jijini Dar es Salaaam.

Kikao hicho cha siku tatu kimefunguliwa tarehe 27 Februari, 2024 jijini Dar-es-Salaam na Mkurugenzi wa Elimu ya Juu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof Peter Msoffe ambapo alizisisitiza Taasisi  zinazotekeleza mradi huo kutumia wataalamu kutoka wizarani ili kufanikisha utekelezaji wa mradi kwa kuzingatia taratibu za Benki ya Dunia.

Waratibu wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) kutoka katika Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela wakishiriki kikao cha Kikanuni cha mradi Februari  27,2024 jijini  Dar es Salaaam.

Katika kikao hicho, Naibu Makamu Mkuu wa Taasisi Mipango Fedha na Utawala na Mratibu wa Mradi, Profesa Suzana Augustino ameeleza kuwa, mpaka sasa taasisi imeshatekeleza mradi kwa asilimia 30 kwa kuzingatia maeneo muhimu ya mradi katika taasisi ikiwepo kuhuisha vifaa vya maabara, kusomesha  na kujenga uwezo kwa wafanyakazi pamoja na kuuhisha mitaala.

Profesa Suzana ametoa wito kwa taasisi zinazotekeleza mradi huo kutumia fedha walizopangiwa kwa usahihi ili kufikia malengo ya mradi kwa maendeleo ya elimu ya juu na taifa kwa ujumla.

 

Taarifa ya utekelezaji wa mradi wa HEET katika Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela iliwasilishwa na Mratibu Msaidizi wa mradi, Bw. Daniel Fisso.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi