Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

UNWTO Kuweka Mikakati ya Kwajengea Uwezo Wadau wa Utalii Nchini Tanzania
Sep 03, 2021
Na Jacquiline Mrisho

Na Mwandishi Wetu Maalum Kisiwa cha Sal-Cape Verde

Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masula ya Utalii Duniani (UNWTO) limeahidi kushirikiana na Tanzania katika kuweka mikakati bora ya kuwajengea uwezo  watu waliopo katika sekta ya utalii nchini kuanzia mwezi juni 2022

Hatua hiyo inakuja kufuatia hali mbaya ya ugonjwa wa COVID  kuidhoofisha sekta ya utalii nchini na Duniani kwa ujumla huku  Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ikikadiriwa kupata hasara ya dola 4.8 bilioni za Marekani (zaidi ya Sh. trioni 11) kwenye sekta ya utalii kutokana na janga la  Corona huku watu milioni 21 wakikosa ajira

Akizungumza na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro katika kikao cha pembeni mwa mkutano wa UNWTO  wa 64 wa Kanda ya Africa ukilenga kufungua fursa za uwekezaji katika sekta ya utalii hasa katika kipindi ambacho sekta ya utalii inachechemea kutokana na kushambuliwa na ugonjwa wa Corona    Katibu Mkuu wa UNWTO Zurab Pololiskashvil  amesema mafunzo hayo yatatolewa kwa Wadau wa Utalii na ili waweze kuendana na janga la Corona katika kuendesha shughuli za utalii nchini

Mkutano huo wa UNWTO wa 64 wa Kanda ya Afrika unafanyika kwa muda wa siku nne kuanzia jana  katika kisiwa cha SAL nchini Cape Verde ambapo umewakutanisha mawaziri 30 wa utalii Barani Afrika ukilenga kujadili mustakabali wa utalii barani Afrika na Duniani kwa ujumla kufuatia uwepo wa janga la ugonjwa wa Corona

 Kat Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo  unaongozwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt.Damas Ndumbaro  akiwa na maofisa na Makamishna Uhifadhi kutoka TFS na TAWA, maofisa pamoja na Balozi wa Tanzani nchini Ufaransa Mhe, Samuel Shelukindo.

Aidha, Katika kikao hicho Katibu Mkuu amesema  mafunzo hayo yatazilenga jamii zinazozunguka vivutio vya utalii ili kuzijengea uwezo wa kushiriki moja kwa moja katika shughuli za  utalii nchini likiwa lengo ni kutengeneza ajira nyingi zaidi kupitia sekta hiyo.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu huyo amemueleza Waziri Dkt.Ndumbaro kuwa UNWTO  iko mbioni kuandaa kalenda  ya mwaka ya UNWTO  ambapo Tanzania nayo itakuwepo ktk orodha hiyo ya  kuendana na matukio yatakavyopangwa katika mkutano huo

Amesema moja ya kipaumbele cha UNWTO kwa sasa ni kuitangaza Tanzania na Africa kwa ujumla

Akizungumza katika kikao hicho cha ana kwa ana na Katibu Mkuu huyo, Dkt.Ndumbaro amesema mafunzo hayo yatatoa matumaini kwa Wadau wa Utalii nchini baada ya ugonjwa wa Corona kuwatikisa

Hata hivyo, Dkt.Ndumbaro amemueleza Katibu Mkuu huyo kuwa Tanzania ni nchi ya kwanza Afrika kwa kufanya vizuri katika  shughuli za Uhifadhi lakini  katika suala la kujitangaza na kutafuta masoko ya utalii imekiwa haifanyi vizuri hivyo ujio wa mafunzo hayo yataiwezesha Tanzania kufanya vizuri katika nyanja hiyo.

Aidha, Dkt.Ndumbaro amemualika Katibu Mkuu wa UNWTO,  Zurabu Pololikashvil kuja kutembelea vivutio volivyopo Tz na kusisitiza kuwa ataambatana naye katika ziara hiyo ya kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo nchini.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi