Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Tuzo ya Rais Samia kutoka CAF Yawasili Nchini
Nov 21, 2025
Tuzo ya Rais Samia kutoka CAF Yawasili Nchini
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa akiwa amewasili kutoka Rabbat nchini Morocco alipokwenda kukabidhiwa Tuzo maalumu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Shrikisho la Mpira wa Mguu Barani Afrika (CAF) Novemba 19, 2025 ikiwa ni kutambua mchango wake katika maendeleo ya michezo nchini.
Na Mwandishi Wetu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, amerejea nchini akiwa na Tuzo maalumu ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.  Samia Suluhu Hassan, aliyokabidhiwa na Shrikisho la Mpira wa Mguu Barani Afrika (CAF) Novemba 19, 2025 Rabbat, Morocco ikiwa ni kutambua mchango wake  katika maendeleo ya  michezo nchini.

Katibu Mkuu Msigwa amewasili leo Novemba 21, 2025 ambapo kupitia tuzo hiyo, Tanzania imetambuliwa kama miongoni mwa mataifa yanayopiga hatua kubwa katika kukuza, kuimarisha na kuendeleza soka la ushindani katika ngazi za vijana, wanawake na ligi za ndani na katika mashindano  makubwa yanayohusisha timu za Taifa.

Akizungumza mara baada ya kuwasili Msigwa alisema “Tuzo hiyo si ya Mhe Rais pekee yake, ni ya Watanzania wote. Na ni matokeo ya umoja, juhudi na imani katika kuendeleza michezo.

"CAF wametutambua kwa sababu tuna safari ya maendeleo inayoonekana,” amesema  Msigwa.

Ameongeza kuwa, Serikali itaendelea kusimamia mageuzi ya michezo, hususan kandanda, ili kuhakikisha Tanzania inaendelea kupaa kimataifa na kutoa nafasi kwa vijana wenye vipaji kuonesha uwezo wao.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi