Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa ya Uteuzi
Aug 19, 2020
Na Msemaji Mkuu

Ikulu, Chamwino.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Joseph Constantine Mafuru kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Mkoani Dodoma.


Kabla ya uteuzi huo, Bw. Mafuru alikuwa Mkuu wa Idara ya Ardhi, Mipango Miji na Maliasili wa Jiji la Dodoma.


Bw. Mafuru anachukua nafasi ya Bw. Godwin Kunambi.


Uteuzi wa Bw. Mafuru unaanza leo tarehe 19 Agosti, 2020.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Chamwino
19 Agosti, 2020

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi