Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Aug 31, 2018
Na Msemaji Mkuu

MAANDALIZI YA MICHEZO YA SHIMIWI 2018

         Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) limeandaa Michezo kwa Watumishi wa Seriali kutoka katika Wizara, Idara Zinazjitegemea, Wakala wa Serikali na Ofisi za Wakuu wa Mikoa itakayofanyika Jijini Dodoma kuanzia tarehe 25 Septemba  hadi 06 Oktoba, 2018  katika Viwanja vya Jamhuri na Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM).

Michezo hiyo itakayoshindaniwa ni  Mpira wa Miguu (Wanaume), Netiboli (Wanawake), Kuvuta Kamba (Wanaume na Wanawake), Riadha (Wanaume na Wanawake), Baiskeli (Wanaume na Wanawake),  Karata (Wanaume na Wanawake), Bao (Wanaume na Wanawake), Drafti (Wanaume na Wanawake) na Darts (Wanaume).          Usajili wa Wachezaji watakaoshiriki katika michezo hiyo tayari umeshaanza tarehe 1 Agosti, 2018  na utamalizika leo 31 Agosti, 2018. Vilabu vinaendelea kuthibitisha ushiriki wao kwa kutaja aina ya Michezo watakayoshiriki zoezi ambalo litafungwa ifikapo tarehe 15 Septemba, 2018.

Ratiba ya michezo ya Ufunguzi ni kama ifuatavyo:-

Kamba Wanaume: Bingwa mtetezi Ofisi ya Rais Ikulu vs MSD.

Kamba wanawake: Bingwa mtetezi RAS Iringa vs Viwanda.

Mpira wa Miguu: Bingwa mtetezi Wizara ya Elimu vs Ukaguzi (NAO).

Netboli: Bingwa mtetezi Menejimenti ya Utumishi  wa Umma vs RAS Manyara.

          Shirikisho linaviomba Vilabu vyote kujianda kikamilifu na kukamilisha taratibu za ushiriki mapema ili kuondoa usumbufu usiokuwa wa lazima. Aidha, tunawaomba wananchi wote wakazi wa Jiji la Dodoma kujitokeza kwa wingi viwanjani kushuhudia Michezo hii ambayo kwa mara ya mwisho katika Mkoa huu ilifanyika mwaka 2013. Hii ni burudani pekee iliyoandaliwa kwa ajili ya wakazi wa Jiji la Dodoma.

           Imetolewa leo Tarehe 31 Agosti, 2018                                   0754 - 763140

Moshi Y. Makuka

KATIBU MKUU – SHIMIWI

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi