Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Aug 30, 2018
Na Msemaji Mkuu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, atafanya ziara ya kikazi katika mikoa ya Mwanza, Mara na Simiyu kati ya tarehe 03 Septemba, 2018 na tarehe 10 Septemba, 2018.

Katika ziara hiyo Mhe. Rais Magufuli ataweka mawe ya msingi na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo, pamoja na kuzungumza na wananchi katika mikutano ya hadhara.

Taarifa zaidi kuhusu ziara ya Mhe. Rais Magufuli katika mikoa husika zitatolewa na viongozi wa mikoa hiyo.

Aidha, baada ya kumaliza ziara katika mikoa hiyo Mhe. Rais Magufuli anatarajia kufanya ziara katika mikoa ya Katavi, Rukwa, Songwe na Mbeya katika tarehe zitakazopangwa.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Chato, Geita

30 Agosti, 2018

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi