Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Rita Yawarahisishia Uhakiki wa Vyeti Waombaji Mikopo ya Elimu ya Juu.
Aug 09, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_8773" align="aligncenter" width="750"] Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) Bi. Emmy Hudson akifafanua kuhusu zoezi la uhakiki wa vyeti kwa wanafunzi watakao omba mkopo mwaka huu (katikati). Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESBL) Bw. Abdulrazaq Badru na Afisa Usajili Muandamizi kutoka RITA, Bw. Adam Mkolabigawa (kulia).[/caption]

Agness Moshi

Wakala wa Usajili, Ufilisi  na Udhamini  (RITA) wameandaa utaratibu maalumu  utakaowawezesha wanafunzi wanaoomba mikopo ya elimu ya juu  kwa mwaka 2017/2018 kufanya uhakiki wa nyaraka mbalimbali kwa urahisi zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Kaimu Mtendaji Mkuu (RITA) Bi. Emmy Hudson    amesema kuwa  uhakiki wa vyeti vya kuzaliwa na vifo unaotumika sasa utawezesha zoezi hilo kufanyika kwa haraka na ufanisi zaidi tofauti na ilivyokuwa miaka iliyopita ambapo wanafunzi wataweza kufanya maombi ya mikopo kwa wakati.

 “ Tumeandaa dawati maalum kwa wanafunzi watakao kuja kuhakiki vyeti vyao  kupitia ofisi za wilaya ambazo awali  zilizotoa vyeti hivyo au  RITA makao  makuu  na kwa walio mbali  na vituo hivyo wanaweza kuhakiki kupitia tovuti maalum ijulikanayo kama uhakiki@rita.go.tz” , alisema Bi.Hudson.

Ameongeza  kuwa, wanafunzi watakao kwenda kufanya uhakiki wanatakiwa wahakikishe wana nakala  za nyaraka zinazosomeka vizuri ikiwa ni pamoja na risiti ya malipo ambayo watalipa kupitia Benki ya NMB akaunti  namba 20610009881 yenye jina la ‘Administrator General Collection Account’.

“ Ili zoezi la uhakiki kwa mwanafunzi likamilike atahitajika awe  na nakala  za nyaraka pamoja na risiti ya ada ya uhakiki  inayolipiwa  shillingi elfu tatu ,  utaratibu huu ni kwa wanafunzi wote  hata watakaohakiki  kwa kupitia tovuti” , alifafanua Bi.Hudson.

Aidha, Bi.Hudson aliwatahadharisha  wanafunzi kujiepusha na udanganyifu wa aina yoyote ile kwenye zoezi hilo wakijihusisha na vitendo vya kughushi nyaraka hizo   watawajibishwa kwa kukiuka sheria za uombaji mikopo.

“ Kuna wanafunzi wanaua wazazi wao ili waweze kupata mikopo, huu ni udanganyifu inabidi waache kwani tutawashugulikia kwa sheria na niwataadharishe wanaotengeneza vyeti kupitia mashirika ambayo hayatambuliki kuacha hiyo tabia mara moja, mwaka jana tulibaini vyeti feki takribani 500 na tulifikisha taarifa hiyo kwenye vyombo vya dola ili wachukuliwe hatua”,aliongeza Bi.Hudson.

Ametoa rai kwa wananchi ambao watoto wao wanaendelea na masomo kufanya usajili na uhakiki mapema badala ya kusubiri  tukio fulani ambalo litawalazimisha kufanya shughuli hizo. Hatua hii itawasaidia kuepusha usumbufu kwao na taasisi ya RITA.

Hata  Bi.Hudson amefafanua kuwa  uhakiki utakaofanywa na RITA utahusisha Tanzania Bara tu na si Tanzania visiwani, aliwataka  wanafunzi wa  Visiwani wafanye uhakiki kupitia ofisi zilizopo Visiwani humo.

Naye , Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo Ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu(HESBL) ,Bw.Abdul-Razaq  Badru amesema kuwa Bodi imefungua rasmi  dirisha la uombaji mikopo kwenye tovuti zao kwa mwaka 2017/2018 tarehe 6 Agosti, na litafungwa tarehe 4, Septemba mwaka huu.

“Tumetoa mwongozo  na vigezo kwa waombaji kwenye tovuti yetu ikiwa na vigezo vya mwombaji  ambapo anatakiwa  kuwa Mtanzania  na awe ameomba kudahiliwa na Chuo Kikuu au Taasisi ya juu inayotambulika na Serikali. Aidha atatakiwa kuambatanisha  vyeti vikiwemo vya taaluma, kuzaliwa na vifo ambavyo vimekwisha fanyiwa uhakiki na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA)” alisema Bw.Badru.

Aliongeza kuwa mwombaji mkopo sharti  ahakikikishe ana anyaraka mbalimbali ikiwemo fomu ya maombi iliyosainiwa na Kamishna wa viapo, nakala za vyeti vya taaluma na nakala za vyeti vya kifo kama  ni yatima.Endapo mwombaji alipata ufadhili anatakiwa kuwa na nakala kutoka katika taasisi iliyomfadhili.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi