Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Rio Ferdinand awasili nchini kwa mwaliko wa Makonda.
May 19, 2026
Rio Ferdinand awasili nchini kwa mwaliko wa Makonda.
Nyota wa zamani wa Leeds, Manchester United na England Bw. Rio Ferdinand, amewasili nchini leo kwa ziara ya siku nne ya mwaliko wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda.
Na Grace Semfuko - MAELEZO

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda ampokea Nyota wa zamani wa Leeds, Manchester United na England Bw. Rio Ferdinand, ambaye amewasili nchini leo Mei 19, 2026, kwa ziara ya siku nne ya mwaliko wa Mhe. Makonda.

Katika mapokezi hayo, Mhe. Makonda aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa na Viongozi wengine wa Wizara hiyo

Katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Terminal 3, maelf ya mashabiki wa soka wamejitokeza kumlaki nyota huyo wa zamani ambaye amesema hakutegemea kupata mapokezi makubwa namna hiyo.

"Tanzania ni nchi nzuri sana, nimepata mapokezi makubwa, sikutegemea kupata mapokezi namna hii, nitawaonesha watu uzuri wa Tanzania na vivutio vyake" amesema Nyota huyo.

Nae Waziri Makonda amesema ujio wa mgeni huyo ni faraja kubwa kwa nchi kwani kutaitangaza Tanzania katika nyanja za burudani na Utalii masuala ambayo Serikali ya Dktw. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa akiyaunga mkono.

Ziara ya Ferdinand inatajiwa kujumuisha shughuli mbalimbali ikiwepo kutembembelea vituo vya michezo vya Vijana (Academies), kukutana na wadau wa michezo pamoja na shughuli za Utalii.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi

slot gacor