Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Rais Samia: Sitachoka Kunyoosha Mkono wa Maridhiano
Nov 14, 2025
Rais Samia: Sitachoka Kunyoosha Mkono wa  Maridhiano
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akikagua gwaride la heshima lililoandaliwa na Jeshi la Polisi mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma tarehe 14 Novemba, 2025.
Na Mwandishi Wetu - Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewakaribisha wadau wa kisiasa kukaa meza moja kwa ajili ya kupata maridhiano ili kujenga mazingira ya mwafaka kwa maendeleo ya Taifa.

Amesema hayo leo Novemba 14, 2025 wakati akizindua  Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jijini Dodoma, tukio  lililohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa,  mabalozi, waheshimiwa wabunge, viongozi wa vyama vya siasa, watendaji wa Serikali na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.


"Sitachoka kunyoosha tena mkono wa maridhiano. Ni matumaini yangu kuwa wadau wa kisiasa wataupokea kwa dhati mkono wa maelewano kupitia Tume ya Usuluhishi na Maelewano ili kwa 
pamoja tujenge mazingira ya muafaka kwa maendeleo ya Taifa letu", amesema Rais Samia.

Ameeleza kuwa kama Taifa  tunajifunza na kurekebisha makosa na mapungufu ya taasisi zetu za kidemokrasia ili misingi yetu ya amani na utulivu iendelee kudumu.

Rais Samia amesema Tanzania ina uzoefu wa miongo mingi ya kuendesha demokrasia katika misingi ya amani, hivyo akiahidi kuendelea kuboresha ustawi wa taifa kulingana na mazingira na wakati.

"Ni jukumu letu sasa kujielekeza kwenye maboresho hayo kwa utashi wetu bila shinikizo lolote.  Naendelea kuwakaribisha vyama vya siasa, vyama vya Kijamii, Sekta binafsi na hata Jumuiya za Kimataifa ili kwa pamoja tuijenge Tanzania", amesema Rais Samia.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi