Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Rais Samia Ahitimisha Ziara Yake Ethiopia, Akutana na Watanzania
Feb 15, 2026
Rais Samia Ahitimisha Ziara Yake Ethiopia, Akutana na Watanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Innocent Shiyo, pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia.
Na Mwandishi Wetu

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amehitimisha ziara yake ya kikazi ya siku nne nchini Ethiopia kwa kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Februari 14 na 15, 2026.

Katika mkutano huo, Rais Samia alijumuika na viongozi wa nchi mbalimbali za Afrika kujadili masuala ya maendeleo ya bara, kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kushughulikia changamoto zinazoikabili Afrika.

Mara baada ya kukamilisha ziara yake ya kikazi, alikutana na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Innocent Shiyo, pamoja na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini humo na kuwapongeza kwa kuendelea kuiwakilisha vyema Tanzania na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Ethiopia.

                   
.
Aidha, Rais Samia alikutana na viongozi wa Diaspora na Watanzania wanaoishi nchini Ethiopia akiwasisitiza umuhimu wao katika kuchangia maendeleo ya Taifa wakiwa nje ya nchi.

Ziara hiyo ni sehemu ya juhudi za Tanzania kuendelea kushiriki kikamilifu katika majukwaa ya kimataifa na kuimarisha nafasi yake ndani ya Umoja wa Afrika

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi