Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Rais Museveni Aipongeza Tanzania kwa Kuleta Mwamko wa Kiuchumi Afrika Mashariki
Nov 29, 2021
Na Jacquiline Mrisho

“Usafirishaji wa mizigo kwa njia ya treni kwa kutumia treni za kisasa utarahisisha zaidi na kuokoa muda, safari moja ya treni itakua na uwezo wa kusafirisha Tani 10,000", amesema Kadogosa.

Aidha, Kadogosa amesema kuwa TRC imeweza kurejesha huduma ya usafirishaji wa shehena ya mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Kampala nchini Uganda kupitia reli, pia TRC inaendelea na jitihada za kuboresha huduma za usafiri wa reli kati ya Tanzania na Uganda kwa kushirikiana na Shirika la Reli Uganda kwa lengo la kuzifaidhisha nchi ya Uganda na Tanzania kupitia Bandari.

“Hivi karibuni miezi miwili iliyopita tumeanza biashara ya mafuta, yanatoka bandari ya Dar es Salaam yanapita ziwa Victoria na kufika Port Bell nchini Uganda, na mpaka sasa tumeshapeleka matenki 72 ambayo ni sawa na lita milioni 3,240,000, ni huduma ambayo ilipotea na tumerudisha”

Kadogosa amesema kuwa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kipande cha Dar es Salaam – Morogoro umefika zaidi ya 95%, Morogoro – Makutupora ambao umefika 75% pamoja na Isaka - Mwanza ambao umefika 3.87%, huku vipande vya Makutupora – Tabora na Tabora – Isaka vikiwa kwenye maandalizi kwa ajili ya kuanza utekelezaji wake.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi