Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

MKUTANO WA MAWAZIRI WA AFYA NA UKIMWI, SADC KUJADILI NAMNA YA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA
Oct 29, 2019
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_48416" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akifafanua jambo kwa Waandishi wa Habari (Hawapo pichani) kuhusu Mkutano wa Mawaziri wa Afya na Ukimwi kwa nchi za SADC, utakaofanyika kuanzia Novemba 04 hadi 08, 2019 katika ukumbi wa Banki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es Salaam.[/caption]

Na.Paschal Dotto

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Mawaziri wa Sekta ya Afya na UKIMWI kutoka Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaotarajiwa kufanyika nchini kuanzia Novemba  04 hadi 08, 2019, katika  Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika Mkutano na Waandishi wa Habari, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe.Ummy Mwalimu amesema kuwa Mkutano huo utafunguliwa rasmi na  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, huku kauli mbiu yake ikiwa ni “Ushirikiano wa nchi za SADC ni nguzo kuu kufikia Maendeleo Endelevu ya Sekta ya Afya na Mapambano dhidi ya UKIMWI.

[caption id="attachment_48419" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu, kwa Waandisahi wa Habari na Wataalmu wa Afya Kutoka Wizara ya Afya (Hawapo pichani) kuhusu Mkutano wa Mawaziri wa Afya na Ukimwi kwa nchi za SADC, utakaofanyika kuanzia Novemba 04 hadi 08, 2019 katika ukumbi wa Banki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es Salaam, kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari-MAELEZO(Uratibu-Mawasiliano Serikalini) Bi. Zamaradi Kawawa wa (kwanza) na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Dkt. Zainabu Chaula.[/caption]

Mhe. Ummy amesema kuwa katika Mkutano huo ambao kwa kiasi kikukubwa utawakutanisha Mawaziri wa Afya na Watendaji Wakuu wa Idara za Afya kutoka Nchi Wanachama wa SADC takribani 200 utakuwa na lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayoikumba sekta ya Afya Ukanda huo wa Afrika.

“Mkutano wa Mawaziri wa Sekta ya Afya na UKIMWI unalenga kuangalia hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa Itifaki ya Afya ya SADC ya mwaka 1999 na Mpango Mkakati wa Kanda kuhusu masuala ya Afya, na pia kutakuwepo na ajenda za kuwezesha ujenzi mpya wa Sekta ya Afya kwa Nchi Wanachama”, Alisema Waziri Ummy.

Alizitaja ajenda hizo kuwa ni  pamoja na Magonjwa ya kuambukiza yanayoziathiri nchi za SADC kama vile Kifua Kikuu, Malaria na UKIMWI; Masuala ya lishe hususani uongezaji virutibisho na lishe ya makuzi kwa watoto, uzito uliopitiliza na viribatumbo na huduma ya Lishe wakati wa majanga

[caption id="attachment_48420" align="aligncenter" width="750"] Mtaalamu wa Chakula na Lishe kutoka Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Grace Moshi akieleza jinsi hali ya lishe duni inavyosababisha viribatumbo na utapiamulo kwa watoto na watu wazima, moja ya Ajenda itakayojadiliwa kwenye Mkutano wa Mawaziri wa Afya na Ukimwi kwa nchi za SADC, utakaofanyika kuanzia Novemba 04 hadi 08, 2019 katika ukumbi wa Banki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es Salaam.[/caption]

Ajenda nyingine ni uimarishwaji wa Mifumo ya Afya ikiwemo uimarishaji wa upatikanaji wa dawa, na upatikanaji wa takwimu za afya, rasilimali watu, rasilimali fedha na Masuala ya ununuzi wa pamoja wa dawa na vitendanishi ili kuongeza ufanisi na kupunguza gharama za manunuzi kwa nchi wanachama, na hiyo itasaidia kuimarishwa kwa Sekta ya Afya huku Tanzania ikiwa mbele kwenye masuala ya ununuzi wa dawa baada ya Bohari Kuu ya Dawa(MSD) kuchaguliwa kuwa mzabuni katika  ununuzi wa dawa kwa nchi za SADC.

[caption id="attachment_48421" align="aligncenter" width="750"] Mtaalamu wa Mpango wa Kudhibiti UKIMWI kutoka Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Zeye Masunga, moja ya Ajenda itakayojadiliwa kwenye Mkutano wa Mawaziri wa Afya na Ukimwi kwa nchi za SADC, utakaofanyika kuanzia Novemba 04 hadi 08, 2019 katika ukumbi wa Banki Kuu ya Tanzania Jijini Dar es Salaam.[/caption]

Aidha Waziri Ummy alisema kuwa katika kuimarisha afya ya Mama na Mtoto suala la kuimarisha huduma za Afya kwa uzazi salama pamoja na chanjo ya mtoto ni suala lingine ambalo linazikumba nchi hizo, kwa hiyo mjadala utajikita katika  suala hilo ili kulinda Afya ya Mama na Mtoto hilo.

Kwa upande wa magonjwa ya mlipuko, majanga ya dharura ikiwemo  magonjwa ya milipuko kama vile Ebola ambayo tayari yanazikumba nchi wanachama kama vile Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Uganda masuala haya yatajadiliwa kwenye mkutano ili kupata ufumbuzi zaidi.

“Wizara yangu ikiwa ni Mwenyekiti wa Mkutano huu itasimamia hoja zake katika masuala mbalimbali ya afya ikiwa ni pamoja na kuzishauri nchi wanachama kuwekeza katika afya bora ambayo ndiyo msingi wa maendeleo na ukuaji wa uchumi; nchi wanachama kuendelea kukabiliana na magonjwa yanayozuilika na nchi wanachama kuwa na huduma za afya zenye usawa kwa watu wote”, Alisema Waziri Ummy.

Mbali na kushiriki Mkutano huo, Mawaziri watapata fursa ya kufanya ziara katika maeneo ya kimkakati ikiwemo; Kiwannda cha Viuadudu vya Malaria cha Labiofam kilichopo Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani tarehe 8 Novemba 2019,  lengo la ziara hiyo ikiwa ni kuzindua rasmi siku ya Malaria ya SADC na Kampeni ya Kitaifa ya Kupambana na Malaria inayojulikana kama “Zero Malaria Starts with me pamoja na kukitangaza kiwanda hicho kwenye nchi wanachama wa SADC ili kupata soko la dawa zinazozalishwa kiwandani hapo, pia watatembelea Bohari Kuu ya Dawa (MSD) kufuatia ushindi wake wa zabuni ya ununuzi, utunzaji,na Usambazaji dawa na vifaa Tiba wa Nchi wanachama wa SADC.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi