Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mhe. Gekul Asisitiza Mazoezi kila Jumamosi ya Mwisho wa Mwezi
Dec 11, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Na Shamimu Nyaki

Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe.Pauline Gekul amesisitiza jamii kutekeleza maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kufanya mazoezi  kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi.

Mhe. Gekul amesema hayo wakati alipokua Mgeni Rasmi  kwenye mashindano ya mbio mjini Moshi ya  Mr UK Marathon yaliyofanyika wilayani hapo Desemba 11, 2022 mkoani Kilimanjaro na  kusisitiza kuwa mazoezi yanaimarisha afya, yanajenga uhusiano na upendo.

"Nawasisitiza Wananchi kuendelea kutekeleza agizo la Mhe. Rais Samia la kufanya mazoezi ili kuimarisha afya zetu na kujikinga na maradhi yasioambukiza, ili tuwe na afya njema tuweze  kufanya shughuli za kuongeza kipato cha Jamii na Taifa letu", amesisitiza Mhe. Gekul.

Mhe. Gekul amewaasa Wandaaji wa Marathon mbalimbali na mabonanza nchini kushirikisha wazee, walemavu, na watoto ili nao washiriki kama ilivyo kwa vijana kwa sasa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mjini, Mhe. Abbasi Kayanda amesema marathon hiyo imesaidia Wananchi wa Moshi kuhamasika kufanya mazoezi pia imeinua uchumi wao na kutoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kufanya mabonanza mengine ya michezo.

Marathon hiyo imeshirikisha mbio za KM 10, 5 na 2 kwa wanaume na wanawake ambapo washindi wamepatiwa Medali na zawadi mbalimbali

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi