Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mhagama: Ungeni Mkono Jitihada Za Serikali
Oct 24, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_37333" align="aligncenter" width="1000"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akisalimiana na Mkurungezi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la UNICEF, Nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Leila Pakkala alipomtembelea ofisini kwake Bungeni Dodoma, Oktoba 24, 2018.[/caption]

 

Na: Mwandishi Wetu

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Jenista Mhagama ameiomba UNICEF kuunga mkono jitihada za Serikali katika programu ya ukuzaji ujuzi nchini inayolenga kuwawezesha vijana kupata ujuzi utakaowawezesha kujiajiri.

Mhe. Mhagama ameyasema hayo leo Jijini Dodoma alipokutana na   Mkurugenzi wa UNICEF nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Leila Pakkala.

[caption id="attachment_37334" align="aligncenter" width="822"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na ujumbe wa wakilishi kutoka UNICEF walipomtembelea Jijini Dodoma, Oktoba 24, 2018.[/caption] [caption id="attachment_37335" align="aligncenter" width="1000"] Mkurungezi Mkazi wa UNICEF, Nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Leila Pakkala akizungumza na Mhe. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu) Jenista Mhagama walipomtembelea Jijini Dodoma.[/caption]

"Ninaomba UNICEF izidi kunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano katika masuala yanayowahusu vijana na watoto ili tuandae kizazi hiki kwa majukumu makubwa ya kitaifa, kwani hawa ndio taifa la kesho" alisema Mhagama

Waziri Mhagama ameishukuru UNICEF kwa kushirikiana na Serikali katika kushughulikia kwa pamoja masuala ya Afya, Elimu, mapambano dhidi Ukimwi na ajira za utotoni.

[caption id="attachment_37336" align="aligncenter" width="900"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana Ajira na Watu Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akimsikiliza Mkurungezi Mkazi wa Shirika la Kimataifa (UNICEF) Nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Leila Pakkala alipomtembelea Jijini Dodoma Oktoba 24, 2018.[/caption] [caption id="attachment_37337" align="aligncenter" width="1000"] Mkuu wa Sera za Kijamii UNICEF, Bw. Paul Ufford (wa pili kutoka kulia) akimwelezea jambo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana Ajira na Watu Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama kuhusu miradi na programu za UNICEF nchini.[/caption] [caption id="attachment_37345" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu) Jenista Mhagama (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurungezi Mkazi wa Shirika la Kimataifa (UNICEF) Nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Leila Pakkala baada ya mazungumzo yao.[/caption] [caption id="attachment_37339" align="aligncenter" width="1000"] Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa (UNICEF), walipomtembelea hii leo Oktoba 24, 2018 Jijini Dodoma. (Picha Zote Na Ofisi Ya Waziri MkuuKazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu)[/caption]

Kwa upande wake, Mkurungezi Mkazi wa UNICEF Nchi za Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Leila Pakkala amesema kuwa Shirika hilo lina mipango mbalimbali inayolenga kuwainua vijana katika sekta mbalimbali ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuongeza kuwa vijana ndio tegemeo la taifa, hivyo UNICEF itaendeleza ushirikiano na Serikali katika kutekeleza mipango yake.

"Ninaipongeza Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza katika kukuza uhamasishaji kwa vijana na kuwashirikisha kwenye masuala ya kimaendeleo" alisema Bi. Pakkala

UNICEF imekuwa ikishirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi na programu za Kitaifa juu ya masuala mbalimbali ya kijamii na kiuchumi ambayo yameleta manufaa katika nchi.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi