Mmoja wa wajumbe wa Ujumbe wa Chama Cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini Bw. Jerald Chami akisisitiza umuhimu wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini kutumia mbinu za kisasa kuwasiliana na wananchi hasa kuhusu miradi inayotekelezwa na Serikali kwa manufaa ya wananchi katika Halmashuri ya Wilaya ya Songea Vijijini.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Peramiho Bw.Godfrey Chipakapaka akisisitiza kuhusu mikakati ya Halmashuri hiyo kumjengea mazingira wezeshi afisa Habari wa Halmashuri hiyo ili atekeleze majukumu yake kwa weledi na tija kwa maslahi ya wananchi hasa katika kutoa taarifa za miradi ya maendeleo.
Mwakilishi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Casmir Ndambalilo akitoa maelezo kwa Afisa Habari wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Vijijini Bi. Jaclin Moyo kuhusu mifumo inayotumiwa na Idara ya Habari MAELEZO kuwasiliana na wananchi kuhusu miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
Ujumbe kutoka Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini na Idara ya Habari (MAELEZO) ukiongozwa na Bi.Gaudensia Simwanza ukisisitiza jambo kwa Afisa Habari wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Vijijini Bi. Jaclin Moyo (kulia) mara baada ya ujumbe huo kufanya ziara kujionea jinsi maafisa Habari katika Halmashuri ya Wilaya ya Peramiho wanavyotekeleza majukumu yao.
(Picha zote na Idara ya Habari MAELEZO)