Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Matukio Katika Picha Ziara ya Viongozi wa TAGCO na Idara ya Habari MAELEZO Peramiho, Songea
Jul 30, 2018
Na Msemaji Mkuu

Mmoja wa wajumbe wa  Ujumbe wa Chama Cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini Bw. Jerald   Chami akisisitiza umuhimu wa Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini kutumia mbinu za kisasa kuwasiliana na wananchi hasa kuhusu miradi inayotekelezwa na Serikali kwa manufaa ya wananchi katika Halmashuri ya Wilaya ya Songea Vijijini.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Peramiho Bw.Godfrey Chipakapaka  akisisitiza kuhusu mikakati ya Halmashuri hiyo kumjengea mazingira wezeshi afisa Habari wa Halmashuri hiyo ili atekeleze majukumu yake kwa weledi na tija kwa maslahi ya wananchi hasa katika kutoa taarifa za miradi ya maendeleo.

Mwakilishi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Casmir Ndambalilo akitoa maelezo kwa Afisa Habari wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Vijijini Bi. Jaclin Moyo kuhusu mifumo inayotumiwa na Idara ya Habari MAELEZO kuwasiliana na wananchi kuhusu miradi  mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali  katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Ujumbe kutoka Chama cha Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini na Idara ya Habari (MAELEZO) ukiongozwa na Bi.Gaudensia Simwanza ukisisitiza jambo kwa Afisa Habari wa Halmashuri ya Wilaya ya Songea Vijijini  Bi. Jaclin Moyo (kulia) mara baada ya ujumbe huo kufanya ziara kujionea jinsi  maafisa Habari katika Halmashuri ya Wilaya ya Peramiho wanavyotekeleza majukumu yao.

(Picha zote na Idara ya Habari MAELEZO)

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi