Matukio Katika Picha: Mapokezi ya Timu ya Taifa Stars
Jan 08, 2026
Baadhi ya picha za matukio ya mapokezi ya timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Tanzania (Taifa Stars) katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam leo, Januari 08, 2025, kufuatia kuwasili kutoka nchini Morocco walikoshiriki michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).
Na
WHUSM
Katika mashindano hayo, Taifa Stars iliandika historia kwa kufanikiwa kufika hatua ya 16 bora, hatua iliyopokelewa kwa shangwe na furaha kubwa kutoka kwa mashabiki na wadau wa soka nchini.