Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Makamu wa Rais Akutana na Makamu wa Benki ya Dunia
Sep 28, 2021
Na Jacquiline Mrisho

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango hii leo Septamba 28, 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia,  Dkt Hafez Ghanem Ikulu Chamwino mkoani Dodoma.

Katika mazungumzo hayo, Makamu wa Rais, Dkt. Mpango amemuhakikishia Dkt. Ghanem kwamba Tanzania itaendelea kushirikiana na Benki hiyo katika masuala mbalimbali ya kuinua uchumi hapa nchini.

Makamu wa Rais, Dkt. Mpango amesema kwamba Serikali ya Awamu ya Sita imeweka kipaumbele katika kuinua sekta binafsi pamoja na kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji hapa nchini. Amesema mpango wa maendeleo wa miaka mitano umelenga kuinua sekta ya viwanda hapa nchini hivyo serikali itaendelea kushirikiana na sekta binafsi katika kufanikisha hilo.

Aidha, Makamu wa Rais Dkt. Mpango amesema ili kukidhi mahitaji ya sekta binafsi hapa nchini serikali imeweka mkazo katika sekta ya elimu hasa elimu ya ufundi ili kupata wahitimu wenye ujuzi watakaoweza kusaidia kuinua sekta hiyo.

Makamu wa Rais amesema serikali imeendelea kuimarisha utawala bora pamoja na kudhibiti rushwa hapa nchini hivyo kuweka mazingira rafiki ya kutekeleza miradi mbalimbali.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia, Dkt. Hafez Ghanem ametaja maeneo ambayo benki hiyo itashirikiana na Tanzania ambayo ni pamoja na uboreshaji miundombinu, mapambano dhidi ya uviko19 pamoja na kuinua uchumi baada ya janga la Uviko 19.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi