Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimsikiliza Meneja wa RUWASA Wilaya ya Mbulu, Onesmo Mwakasege ambaye alitoa maelezo kuhusu mradi wa maji wa Maghang Juu wilayani Mbulu kabla ya kuzindua mradi huo, Januari 24, 2022. Wa tatu kushoto ni Waziri wa Maji, Juma Aweso na wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Makongoro Nyerere
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizindua mradi wa maji wa Maghang Juu wilayani Mbulu akiwa katika ziara ya Mkoa wa Manyara, Januari 24, 2022. Kushoto ni Waziri wa Maji, Juma Aweso, kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Makongoro Nyerere na wa pili kulia ni Mbunge wa Mbulu Vijijini, Flatei Masay.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Mbunge wa Mbulu Vijijini, Flatei Masay (kulia) wakifurahia baada ya Waziri Mkuu kuzindua mradi wa maji wa Maghang Juu wilayani Mbulu akiwa katika ziara ya Mkoa wa Manyara, Januari 24, 2022. Kushoto aliyebeba ndoo ya maji baada ya uzinduzi ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Maghang, Paulina Petro.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi baada ya kuzindua mradi wa maji wa Maghang Juu wilayani Mbulu akiwa katika ziara ya Mkoa wa Manyara, Januari 24, 2022. Kushoto ni Waziri wa Maji, Juma Aweso.