Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Lugola: Wananchi Epukeni Uchafuzi wa Mazingira.
Oct 30, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_21302" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola akizungumza na waandishi wa habari na wakazi wa eneo la Tande kwa Mtogole wakati wa ziara ya waziri huyo ya kuzindua operesheni ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima.[/caption]

Na:Paschal Dotto

SERIKALI imewataka Wananchi kuzingatia usafi kuwa kusafisha mitaro na kuzibua maji yaliyopo katika mito ili kuepukana na adha ya mafuriko inayosababishwa kuwepo na taka ngumu zinazozuia utiririkaji wa maji kwa urahisi.

Akizungumuza katika uzinduzi wa Operesheni ‘Tudhibiti Uchafuzi wa Mazingira Tusalimike’ Jijini Dar es Salaam,  itakayoanza nchini kote tarehe Novemba Mosi 1 hadi Desemba 30, mwaka huu, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola alisema ili jamii ibaki salama katika mazingira yao ni wajibu wao kuzingatia dhana ya usafi.

[caption id="attachment_21303" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola akikagua eneo la Mto Ng’ombe eneo la Tandale kwa Mtogole wakati wa ziara ya waziri huyo ya kuzindua operesheni ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima.[/caption]

“Uzalishaji wa taka ngumu ambao tumekuwa tukiufanya umesababisha kuziba mifereji ya maji, mitaro, na mito matokeo yake maji yametafuta mahali pakupita yakakosa na kuvamia makazi ya watu na ndiyo maana ya mafuriko huku Manzese Mtogole”, alisema Mhe. Lugola.

Aliongeza kuwa kupitia athari za mafuriko ya maji katika eneo hilo la kwa Mtogole, Wananchi wanapaswa kujifunza kuwa athari ya kutokufanya usafi na kuondoa taka ngumu na jinsi zinavyoweza kuleta athari katika makazi.

[caption id="attachment_21304" align="aligncenter" width="750"] Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola akisafisha eneo la Mto Ng’ombe kuashiria uzinduzi wa operesheni maalum ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima.[/caption] [caption id="attachment_21305" align="aligncenter" width="750"] Eneo la Mto Ng’ombe likiwa limejaa taka ngumu kama zilivyokutwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira Kangi Lugola wakati wa ziara ya waziri huyo ya kuzindua operesheni ya miezi miwili ya kusafisha mito nchi nzima. (Picha na Eliphace Marwa)[/caption]

Aidha Naibu Waziri huyo alitoa wito kwa wananchi kupitia Viongozi wa ngazi za mamlaka za Serikali za Mitaa kufanya kazi ya kuwaelimisha wananchi na kutoa vitendea kazi ikiwemo magari ya kuzolea taka.

“Halmashauri zote za Majiji, Manispaa na Miji pamoja zihakikishe zinawashirikisha Watanzania kwa  asilimia 100 katika oparesheni  Novemba Mosi kwa kuzibua mitaro, mifereji na mito karibu na makazi yao”,alisisitiza Mhe. Lugola.

Naibu Waziri Lugola pia alitoa onyo kwa watendaji wa halmashauri watakaokwepa kushiriki katika operesheni hiyo na kuwaasa kutoa msaada wa hali na mali utaohitaji kutoka kwa wananchi ili kuhakikisha kuwa inabaki Tanzania salama.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi