Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Lowassa Alikuwa Anasimamia Kila Alichotaka Kifanyike
Feb 16, 2024
Lowassa Alikuwa Anasimamia Kila Alichotaka Kifanyike
Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda akiongoza mamia ya wananchi kuaga mwili wa Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Edward Lowassa wakati wa ibada ya kumuaga kiongozi huyo iliyofanyika nyumbani kwake Kijiji cha Ngarash, wilayani Monduli leo Februari 16, 2024.
Na Lilian Lundo - Maelezo

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda amesema Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Edward Lowassa alikuwa kiongozi aliyekuwa anajua kusimamia kile alichokuwa anataka kifanyike.

Mhe. Mizengo amesema hayo leo Kijiji cha Ngarash wilayani Monduli leo Februari 16, 2024 wakati wa ibada ya kumuuga Hayati Lowassa iliyofanyika kijijini hapo, ambaoo ni nyumbani kwa kiongozi huyo.

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda akitoa salamu za pole kwa familia ya Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Edward Lowassa wakati wa ibada ya kumuaga kiongozi huyo iliyofanyika nyumbani kwake Kijiji cha Ngarash, wilayani Monduli leo Februari 16, 2024.

“Alipokuwa Waziri Mkuu nilipata nafasi ya kufanya kazi naye, alikuwa ni kiongozi aliyekuwa anajua kusimamia kile alichokuwa anataka kifanyike, na alikuwa hana utani katika hilo,” amesema Mhe. Mizengo.

Ameendelea kusema kuwa, na hata unapokamilisha kazi fulani alikuwa akihamasisha kupeana hongera badala ya kupeana pole, kwani alikuwa anaamini unapomaliza jukumu fulani unastahili kupewa hongera kwa kukamilisha jambo hilo, na sio kupewa pole.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi, Dkt. Emmanuel Nchimbi akiaga mwili wa  Waziri Mkuu Mstaafu, Hayati Edward Lowassa leo Februari 16, 2024 Kijiji cha Ngarash wilayani Monduli.

Mhe. Pinda amesema Hayati Lowassa amefanya mambo mengi ya kuigwa akiwa mtumishi na mtendaji wa serikali, hivyo amewataka Watanzania kuiga yale mema aliyoyafanya kiongozi huyo na kuyaendeleza.

Hayati Edward Lowassa anatarajiwa kuzikwa Februari 17, 2024 nyumbani kwake Kijiji cha Ngarash kilichopo wilayani Mondulu mkoani Arusha, ambapo Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan atawaongoza Watanzania katika mazishi ya kiongozi huyo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi