Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Kampeni ya Uzalendo na Utaifa
Dec 08, 2017
Na Msemaji Mkuu

LEO ni siku ya Uzinduzi wa kampeni ya Uzalendo na Utaifa. Uzinduzi huo utafanyika katika ukumbi wa Chimwaga Dodoma,  kwa ratiba itakayoanza saa 9 mchana na kuisha saa 3 usiku.. Kati ya matukio yatakayokuweko ni maandamano yatakayoshirikisha wasanii mbalimbali na pia kazi za sanaa, baada ya watu wote kufika na kutulia Chimwaga kutakuweko na wimbo maalumu wa Uzalendo, filamu ya kihistoria, hotuba za viongozi wastaafu, uzinduzi wa kitabu, na kisha Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania atatoa vyeti vya udhamini hatimae chakula. Wimbo hapo juu ni kazi ya wanamuziki Anania Ngoliga na John Kitime wakipiga gitaa na rimba kuisifia nchi yao,

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi