Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

JKCI Yafungua Kliniki Mpya za Matibabu ya Moyo
Feb 26, 2025
JKCI Yafungua Kliniki Mpya  za Matibabu ya Moyo
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Dkt. Peter Kisenge, akizingumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio na mwelekeo wa taasisi hiyo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita leo tarehe 26 Februari, 2025, katika ofisi za Idara ya Habari - MAELEZO, Dodoma.
Na Frank Mvungi, Dodoma

Taasisi ya Moyo  ya Jakaya Kikwete (JKCI) imedhamiria kuwafikia wananchi wengi zaidi kwa kufungua kliniki  mbili mpya za matibabu ya moyo zilizopo Kawe katika jengo la Mkapa Health Plaza na nyingine katika jengo la Osterbay Plaza.

"Huduma tunazotoa  ni uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo kwa watoto na watu wazima, kliniki za mishipa ya  damu, huduma za maabara, mazoezi tiba, huduma ya matibabu majumbani,elimu ya afya, lishe bora  na mafunzo kwa jamii.

Huduma nyingine ni pamoja na matibabu ya magonjwa ya ndani, duka la dawa, tiba mtandao,huduma ya gari la wagonjwa na huduma ya upimaji wa afya kwa vikundi mbalimbali.

Sanjari na hayo, Dkt. Kisenge amesema kuwa Taasisi hiyo ina mikataba na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Madaktari wa Upasuaji Afrika Mashariki, Kati na Kusini mwa Afrika katika kutoa mafunzo bobezi ya matibabu ya moyo kwa wataalamu wa afya, Chuo Kikuu cha Jagiellonian cha Poland na Chuo Kikuu cha New York cha Marekani kwa ajili ya kufanya utafiti,elimu na utoaji wa huduma kwa wagonjwa wa moyo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi