Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Dkt. Shein Azungumza na Uongozi wa Wizara
Oct 28, 2017
Na Msemaji Mkuu

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto  katika  kikao cha siku moja cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja, (Picha na Ikulu 28/10 /2017.)

Waziri wa  Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto  Mhe. Moudline Syrus Castco (katikati) akisoma taarifa yake katika  kikao cha siku moja cha Uongozi wa Wizara  hiyo katika Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja chini ya Mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein (hayupo pichani).  Wengine ni Katibu Mkuu Kiongozi Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee (kulia) na Naibu Waziri Mhe. Shadya Mohamed Suleiman, (Picha na Ikulu. 24/10 /2017.)

Maafisa wa Idara zilizo chini ya Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee,Vijana, Wanawake na Watoto  wakiwa katika  kikao cha siku moja cha Utekelezaji wa Mpango kazi kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka kilichofanyika leo katika ukumbi wa  Ikulu Mjini Unguja na kuongozwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein (hayupo pichani), (Picha na Ikulu 28/10 /2017.)

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi