Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Dkt. Mwakyembe Avipa Wiki Mbili Vilabu vya Mchezo wa Kriketi Kujisajili
Oct 02, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_36125" align="aligncenter" width="800"] Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (Kulia) akifafanua jambo wakati wa mkutano na wadau wa mchezo wa Kriketi alipokutana nao hapo jana katikati ukumbi wa mkutano uliopo Uwanja wa Taifa, kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Yusuph Singo.[/caption]

Na Lorietha Laurence - WHUSM

Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe ametoa wiki mbili kwa vilabu vyote vya mchezo wa Kriketi nchini ambavyo havijasajiliwa  kufika Baraza la Michezo La Taifa kwa ajili ya kujisajili .

Akizungumza na wadau hao wa mchezo huo jana katika Ukimbi wa mikutano  uliopo Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam, Dkt. Mwakyembe ameeleza kuwa ni wajibu wa kila kilabu cha mchezo nchini kufuata sheria na taratibu zinazosimamia sekta ya michezo.

“Kama kuna kilabu chochote cha mchezo wa kikreti kipo na hakijasajiliwa, natoa wiki mbili  kuweza kufuata taratibu na sheria za usajili ili viweze kutambulika kisheria ” alisema Dkt. Mwakyembe.

[caption id="attachment_36127" align="aligncenter" width="800"] Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa Bw. Makoye Nkenyenge (kulia) akizungumza na wadau wa chama cha kriketi Tanzania walipokutana nao jana uwanja wa Taifa wa Michezo, katikati ni Waziri wa Habari ,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe na kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Yusuph Singo (kushoto).[/caption]

Aidha aliongeza kwa kuutaka uongozi wa Chama cha Kriketi Tanzania kuhakikisha unatenga siku moja  kwa ajili ya mkutano na wanachama wake ili kupata nafasi ya kupitia vipengele vinavyounda katiba ya chama hicho kwa ajili ya maboresho mbalimbali.

Vilevile Waziri Dkt. Mwakyembe  alipata fursa ya kusikiliza changamoto mbalimbali  zinazokikabili chama hicho cha mchezo wa Kriketi na kuhaidi kuzifanyia kazi changamoto hizo.

Kwa Upande wake Kaimu Katibu  Mtendaji wa Baraza la Michezo  la Taifa Bw.Makoye  Nkenyenge amewataka wanachama hao kufanyia kazi maagizo yaliyotolewa na Waziri Dkt. Mwakyembe kwa kuhakikisha wanasajili vilabu vyote ambavyo havijasajiliwa.

[caption id="attachment_36128" align="aligncenter" width="800"] Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Yusuph Singo (kushoto) akieleza jambo kwa wadau wa chama cha kriketi Tanzania walipokutana nao jana uwanja wa Taifa wa Michezo, katikati ni Waziri wa Habari ,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe na kulia ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa Bw. Makoye Nkenyenge.[/caption] [caption id="attachment_36126" align="aligncenter" width="800"] Wadau na wanachama wa chama cha Kriketi Tanzania wakifuatilia kwa makini majadiliano yaliyokuwa yakiendelea baina yao na Waziri wa Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe (Hayupo katika Picha), katika kikao kilichofanyika jana uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.[/caption]

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Kriketi Tanzania Bw. Taher Kitisa ameahidi kushirikiana na wanachama wenzake katika kuhakikisha wanapitia katiba ya chama hicho na kuifanyia maboresho.

Dkt. Mwakyembe alikutana na wanachama wa Kriketi  zaidi ya 60 lengo ikiwa  ni kujadiliana mambo mbalimbali yanayohusu mchezo huo ikiwemo uboreshwaji wa uongozi wa chama hicho kwa manufaa  ya ustawi wa mchezo huo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi