Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

DAWASA yaiwezesha Bandari ya Dar es Salaam Kupata Maji ya Uhakika
Sep 30, 2018
Na Msemaji Mkuu

Na ; Georgina Misama

Mamlaka ya Maji  Safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) imenza kutekeleza kwa vitendo agizo la Serikali kuimarisha huduma ya maji safi katika Bandari ya Dar es Salaam kwa kuweka Bomba kubwa  zaidi ya lililopo sasa.

Kwa mujibu wa Mamlaka hiyo lengo la upanuzi wa miundo mbinu ya kufikisha maji Bandarini hapo ni kuwezesha meli zote za abiria na mizigo zinazotia nanga kupata huduma hiyo kulingana na mahitaji na kwa wakati wote.

“Kazi hii ya kupanua miundo mbinu ya maji yanayotumika katika Bandari yetu ni maagizo ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa alilolitoa wakati wa ziara yake iliyolenga kutambua wateja wakubwa wa maji Jijini Dar es Salaam”. Inasisitiza sehemu ya taarifa hiyo.

Aidha, Taarifa hiyo imefafanua kuwa kuimarishwa kwa miundo mbinu ya kupeleka maji katika Bandari hiyo kutasaidia kuongeza tija kwa watumiaji wa huduma hiyo katika Bandari hiyo.

Kwa mujibu wa DAWASA dhamira yake ni kuwafikia wananchi wote katika maeneo yao kwa kufikisha huduma ya maji safi na salama kama ilivyo dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano inayosisistiza utoaji wa huduma bora kwa wananchi wote.

DAWASA imekuwa ikitekeleza jukumu hilo kwa kutekleza miradi ya kimkakati katika Jiji la Dar es Salaam na mkoa wa Pwani kwa maslahi ya wanachi  wa maeneo hayo na Taifa kwa ujumla.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi