Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Bodi Tume Ulinzi Taarifa Binafsi Yakabidhiwa Vitendea Kazi
Dec 29, 2023
Bodi Tume Ulinzi Taarifa Binafsi Yakabidhiwa Vitendea Kazi
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Ndg. Mohammed Khamis Abdulla akimkabidhi sheria na kanuni mbili Mwenyekiti wa Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Balozi Adadi Rajabu ikiwa ni nyenzo zitakazoiwezesha tume hiyo kuanza kazi rasmi mnamo Januari, 2024
Na Ahmed Sagaff - Maelezo

Bodi ya Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi imekabidhiwa rasmi vitendea kazi vyenye umuhimu zaidi ili iweze kuanza kazi rasmI.

Akizungumza leo jijini Dodoma mara baada ya makabidhiano hayo,  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Ndg. Mohammed Khamis Abdulla amesema tume hiyo itaanza kazi Januari 2024.

"Leo tumekabidhiana sheria na tumekabidhiana kanuni mbili, hizi ni nyenzo zitakazoiwezesha tume hiyo kuanza kazi rasmi," ameeleza Ndg. Abdulla.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Balozi Adadi Rajabu amefahamisha kuwa nchi jirani tayari zina tume kama hiyo hivyo Watanzania walikuwa wakisubiria kwa hamu kuanzishwa kwa tume hiyo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi