Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Basata Yazindua Chama cha Wanamitindo Tanzania
Jan 31, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_28313" align="aligncenter" width="750"] Mwanzilishi wa Chama cha Wanamitindo Tanzania (FAT) Mustafa Hassanali (kulia) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa chama hicho mapema hii leo jijini Dar es Salaam, katikati ni Katibu Mtendaji toka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mngereza na kushoto ni Mwanamitindo mkongwe nchini Bi. Asia Idarous.[/caption]

Na: Nyakongo Manyama

BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA) kwa kushirikiana na wabunifu wa Tanzania wamezindua Chama cha Mitindo Tanzania (FAT) kitakachowaunganisha wabunifu wote hatua inayolenga kuinua na kuiongezea hadhi sekta ya mitindo nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Katibu  Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa  (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza  amesema sekta ya mitindo nchini ikiimarishwa itaweza kuleta mapinduzi makubwa kwa kuzalisha ajira kwa vijana.

“Katika kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kujenga Tanzania ya viwanda, tasnia ya ubunifu wa mavazi, tumeamua kulima pamba ambayo ndiyo itakayozalisha mavazi, hivyo kusingekuwa na wabunifu hatungekuwa na mavazi yenye utamaduni wa Tanzania” alisema Mungereza

[caption id="attachment_28314" align="aligncenter" width="750"] Katibu Mtendaji toka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Godfrey Mngereza (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa uzinduzi wa Chama cha Wanamitindo Tanzania (FAT) mapema hii leo jijini Dar es Salaam, kulia ni Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi TanzaniaAdrian Nyangamalle na kushoto ni Mwanamitindo mkongwe nchini Bi. Asia Idarous.[/caption]

Aidha Mngereza aliongeza kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazoongoza katika uzalishaji wa ngozi duniani, ambapo katika kutumia fursa hiyo, Chama cha wabunifu Tanzania kimepanga raslimali hiyo kwa kuzalisha  bidhaa mbalimbali ikiwemo viatu, mikanda na mabegi .

Naye mwanzilishi wa chama hicho Bw. Mustafa Hassanali amesema kuwa  lengo la kuanzishwa kwa chama hicho ni katika kukuza, kuimarisha na  kuendeleza sekta ya mitindo Tanzania pamoja na kuwapatia ujuzi, uzoefu wadau wote wa   sekta ya mitindo Tanzania.

Kwa upande wake, Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufundi Tanzania, Adrian Nyangamalle amekipongeza chama hicho na kusema kuwa tasnia ya mitindo imetoa ajira kubwa kwa vijana na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano na jumuiya hiyo ili kutimiza malengo yake kwa haraka.

Aidha Nyangamalle ameongeza kuwa Shirirkisho la Chama cha Ufundi kwa kushirikiana na BASATA wameanzisha mchakato wa kuwatambua wasanii wote nchini kwa kuandaa kanzi data itakayosaidia kufahamu wasanii waliopo nchini ili kuweza kutambulisha mchango wao katika kuinua uchumi.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi