Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Marufuku Kuchambua Bajeti nje ya Mfumo- Maganga
Sep 28, 2020
Na Msemaji Mkuu

Na Daudi Manongi, Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bi Mary Maganga amemwelekeza Msajili wa Hazina kutochambua bajeti yoyote itakayowasilishwa nje ya mfumo wa kielektroniki wa  Planrep.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi Mary Maganga akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya mfumo wa uandaaji wa bajeti-planrep kwa wakala za Serikali,Taasisi na Mashirika ya Umma leo Jijini Dodoma.

Bi Mary ameyasema hayo leo wakati akifungua mafunzo ya Matumizi ya Mfumo Mpya wa Uandaaji na Uwasilishaji wa Bajeti na Taarifa za Bajeti  ki-elektroniki wa PlanRep katika Wakala za Serikali, Taasisi na Mashirika ya Umma jijini Dodoma.

“Ili kuwezesha ufanisi katika usimamizi wa mali za umma, ilihitajika pamoja na mambo mengine kuwa na mifumo madhubuti ya kielektroniki itakayorahisisha usimamizi wa rasilimali hizo”,alisema Bi Mganga.

Msajili wa Hazina Athumani Mbutuka akizungumza na washiriki 944 kutoka Taasisi na Mashirika yote 236 yaliyoko chini ya Ofisi ya Msajili wa Hazina. Mafunzo haya yanafanykia katika vituo vitatu tofauti ambavyo ni Dar es Salaam, Morogoro na Dodoma.

Amesema hadi kufika mwezi Juni mwaka 2019, Serikali ilikuwa imewekeza katika Taasisi,  Mashirika ya Umma na Kampuni zinazomilikiwa na Serikali kwa hisa chache zipatazo  266   zenye uwekezaji wa kiasi cha shilingi trilioni 59.6na kudhihirisha uhitaji wa mifumo ya kielektroniki.

Akieleza faida za mfumo huo, Msajili wa Hazina, Athumani Mbuttuka amesema uwepo wa mfumo huu utasaidia kuimarisha usimamizi wa matumizi ya fedha za umma katika mashirika na taasisi za umma pamoja na upatikanaji wa taarifa za uhakika na kwa wakati; kupunguza gharama kubwa za fedha za umma katika ununuzi, uundaji, usimikaji, uendeshaji na usimamizi wa mifumo hiyo, pamoja kupunguza utitiri wa mifumo ya kibajeti ya kieletroniki iliyoanzishwa bila kupata ridhaa ya Wizara ya Fedha na Mipango ambayo ni msimamizi mkuu wa fedha na mali za umma.

Mafunzo hayo yatashirikisha jumla ya washiriki 944 kutoka katika taasisi na mashirika ya umma 236.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi