Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Makubaliano ya Kuwarejesha Nyumbani Wakimbizi wa Burundi Yatiwa Saini Dar Leo
Aug 31, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_11230" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwigulu Nchemba (Katikati), akisaini hati ya makubaliano ya kuwarejesha makwao wakimbizi wa Burundi waishio Tanzania wakati wa mkutano wa siku moja uliofanyika leo Jijini Dar es Salaa. Kutoka kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi Bw. Pascal Barandagiye, Mkurugenzi wa Huduma za Wakimbizi Tanzania Bw. Harrison Mseke, Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi nchini Tanzania (UNHCR), Bi. Chansa Ruth Kapaya na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi nchini Burundi Bw. Abel Mbilinyi.[/caption]

Na: Mwandishi Wetu , MAELEZO

Tanzania, Burundi na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Wakimbizi (UNHCR) wamepitisha mpangokazi wa kuwarejesha nyumbani wakimbizi raia wa Burundi ambao tayari wamejiandikisha kwa hiari kurejea nyumbani.

Mpangokazi huo ni sehemu ya makubaliano yaliyotiwa saini leo kufuatia Kikao cha 19 cha Kamisheni ya Pande Tatu kilichofanyika jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na mawaziri wanaoshughulikia wakimbizi wa Tanzania, Burundi na mwakilishi wa UNHCR.

[caption id="attachment_11231" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwigulu Nchemba akibadilisha hati ya makubaliano ya kuwarejesha makwao Wakimbizi kutoka Burundi waishio Tanzania na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi nchini Tanzania (UNHCR), Bi. Chansa Ruth Kapaya katika mkutano wa siku moja uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.[/caption] [caption id="attachment_11232" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Mambo ya Ndani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwigulu Nchemba akimsikiliza Mkurugenzi wa Huduma za Wakimbizi Tanzania Bw. Harrison Mseke baada ya kusaini hati za makubaliano ya kuwarejesha makwao wakimbizi wa Burundi waishio nchini Tanzania katika mkutano wa siku moja majadiliano kuhusu urejeshwaji wa wakimbizi hao uliofanyika leo Jijini Dar es Salaam.[/caption]

Chini ya Mpangokazi huo wa kipindi cha karibu miezi mine (07 Septemba hadi 31 Disemba, 2017) wakimbizi 12,000 ambao tayari wamejiandikisha kwa hiari watarejeshwa nyumbani huku ukitoa nafasi kwa wengine zaidi watakaojiandikisha kujumishwa.

Makubaliano hayo yalitiwa saini na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba, Waziri wa Mambo ya Ndani na Elimu ya Uzalendo wa Burundi Pascal Barandagiye na Mwakilishi wa UNHCR nchini Bibi Chansa Ruth Kapaya.

Chini ya Makubaliano hayo shirika la UNHCR na washirika wake wataweza kutembelea maeneo ya mipakani ya Tanzania na Burundi kwa lengo la kusaidia mchakato wa urejeshaji wa hiari wa wakimbizi hao na masuala mengine yanayohusu hifadhi ya wakimbizi na raia wengine wanaohitaji hifadhi.

[caption id="attachment_11233" align="aligncenter" width="750"] Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mwigulu Nchemba (katikati) akiteta jambo na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi nchini Tanzania (UNHCR) Bi. Chansa Ruth Kapaya, kulia ni Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi nchini Burundi (UNHCR) Bw. Abel Mbilinyi na kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani wa Burundi Bw. Pascal Barandagiye na Mkurugenzi wa Huduma za Wakimbizi Tanzania Bw. Harrison Mseke (wapili kushoto) wakati wa mkutano wa siku moja wa kusaini makubaliano ya kuwarejesha makwao wakimbizi kutoka Burundi waishio nchini Tanzania leo Jijini Dar es Salaam. (Picha zote na: Thobias Robert)[/caption]

Pande hizo za makubaliano zimetoa wito kwa Jumuiya ya Kimataifa kutoa ushirikiano katika kutekeleza zoezi la kuwarejesha nyumbani wakimbizi hao na kulitaka shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) kutoa chakula kwa wakimbizi wanaorejea kwa kipindi cha miezi mitatu.

Kikao hicho cha 19 cha Kamisheni ya Pande Tatu kimeeleza kutumbua na kuthamini ukarimu wa watanzania ambao umewezesha mamilioni ya wakimbizi kuishi Tanzania tangu nchi hiyo ilipopata uhuru mwaka 1961 na zaidi kuendelea kuwakarimu wakimbizi wapatao 350,000 miongoni mwao 256,850 wakiwa raia wa Burundi.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi