Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Waziri Mabula Ashiriki Mkutano wa Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe
Jul 13, 2023
Waziri Mabula Ashiriki Mkutano wa Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Angeline Mabula (kulia) akiwa na Mhe. Anthony Mavunde, Naibu Waziri wa Kilimo na Mhe. Deogratius Ndejembi, Naibu Waziri, ofisi ya Rais - TAMISEMI katika Mkutano wa Pili wa Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe unaofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 13 Julai, 2023..
Na Mwandishi Wetu

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Angeline Mabula ameshiriki Mkutano wa Pili wa Baraza la Mawaziri wa Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe uliofanyika leo tarehe 13 Julai 2023 Jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo wa siku moja unaoongozwa na Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Awesu unahusisha viongozi na wataalamu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Malawi huku ujumbe wa Malawi ukioongozwa na Waziri wake wa Maji na Usafi wa Mazingira, Mhe. Abida Sidik Mia.

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (kushoto) akiwa na Waziri wa Maji wa Malawi, Mhe. Abida Sidik Mia katika mkutano wa pili wa Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe unaofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 13 Julai, 2023.

Mawaziri wengine wa Tanzania wanaoshiriki mkutano huo ni Mhe. Anthony Mavunde, Naibu Waziri wa Kilimo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Deogratius Ndejembi na Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato.

Mkutano huo ni muendelezo wa vikao vya pamoja baina ya Serikali ya Tanzania na Malawi unaolenga kuimarisha usimamizi, uhifadhi, uendelezaji na matumizi endelevu ya rasilimali ya maji ya mto Songwe.

Ujumbe wa Malawi ukiwa katika Mkutano wa Pili wa Kamisheni ya Bonde la Mto Songwe unaofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 13 Julai, 2023.

Tanzania na Malawi zilishiriki majadiliano ya pamoja yaliyofanyika mwaka 1976 kuhusu namna bora ya kutatua changamoto zinazosababishwa na Mto Songwe kwa madhumuni ya kutafuta ufumbuzi wa kudumu.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi