Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Waziri  Dkt.Mwakyembe Azindua Kituo cha Radio Jamii cha TBC 92.1 Jijini Arusha
Mar 11, 2018
Na Msemaji Mkuu

[caption id="" align="aligncenter" width="800"] Waziri wa Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati) akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa kituo cha redio Jamii cha Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) chenya masafa ya 92.1 leo Jijini Arusha.[/caption]  

[caption id="attachment_29242" align="aligncenter" width="800"] . Waziri wa Habari ,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiangalia mitambo ya kurusha matangazo katika studio za kituo kipya cha redio Jamii cha TBC chenye masafa ya 92.1 leo Jijini Arusha mara baada ya kukizindu rasmi.[/caption]

Na Lorietha Laurence-WHUSM, ARUSHA

Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe amezindua kituo cha Redio Jamii cha TBC chenye masafa ya 92. 1 ambacho kimegharimu jumla ya milioni 627  leo Jijini Arusha.

 Wakati wa uzinduzi huo  Mhe. Dkt. Mwakyembe  amesema lengo kuu la kuanzishwa kwa kituo hicho cha redio ni kuhabarisha umma wa Arusha na mikoa ya jirani  fursa mbalimbali zinazopatikana katika Jiji hilo ukizingatia chanzo kikuu cha mapato yake yanatokana na Utalii wa ndani.

“Ni matarajio yangu redio hii itakuwa mstari wa mbele katika kutangaza na kueleza fursa mbalimbali zinazopatikana katika Jiji la Arusha pamoja na kuhabarisha umma masuala mbalimbali ya kijamii,kisiasa na kiuchumi” amesema Mhe.Dkt. Mwakyembe

[caption id="" align="aligncenter" width="800"] Waziri wa Habari ,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akiongea na wananchi wa Arusha (hawapo katika picha) katika hafla ya kuzindua kituo cha Redio Jamii cha TBC chenye masafa ya 92.1 leo Jijini Arusha, waliokaa wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Mjumbe wa Bodi ya TBC Dkt. Hassan Abbas, Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Gabriel Daqqaro na wa kwanza kulia ni Mkurugezni wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote Mhandisi. Peter Ulanga na wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC).[/caption]  
[caption id="attachment_29244" align="aligncenter" width="800"] Waziri wa Habari ,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe(kushoto) akimsikiliza Fundi Mitambo wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Bi. Lucy Mgala alipotembelea mitambo ya TBC iliyoko Njiro Jijini Arusha.[/caption]

Aidha ameeleza kuwa TBC kama Shirika la Umma halina budi kuhakikisha inatoa matangazo ya uhakika na ukweli kwa kuifikia jamii kubwa zaidi hususani zile za vijijini ambako vyombo vingine vya habari havijaweza kuwafikia.

Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Gabriel Daqqaro ameushukuru uongozi wa TBC na Serikali kwa ujumla kwa kuona  umuhimu wa  kuwepo kwa kituo cha redio jamii  kwa ukanda wa kaskazini.

“Redio hii ya Jamii ni muhimu sana kwa watu wa Ukanda wa Kaskazini ukizingatia asilimia 80 ya mapato yake yanatokana na sekta ya utalii hivyo itatupa fursa ya kujitangaza zaidi” alisema Bw. Daqqaro.

Kwa upande wake Mjumbe wa Bodi ya TBC na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbas ameeleza kuwa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)  linahitaji uwekezaji mkubwa ili kufika maeneo mengi zaidi nchini.

Vilevile Mkurugenzi  Mkuu Shirika La Utangazaji La Taifa (TBC) Dkt. Ayoub Rioba amesema kuwa Redio jamii iliyofunguliwa rasmi leo Jijini Arusha  ni mkakati wa Serikali kuwafikia wananchi wengi mahali popote walipo.

Habari Mpya

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi