Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Utamaduni wa Kufanya Kazi ni Njia ya Kufikia Lengo la Tanzania ya Viwanda.
Jul 04, 2017
Na Msemaji Mkuu

[caption id="attachment_5394" align="aligncenter" width="750"] Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel(kulia) akiongea na Menejmenti ya Mkoa wa Songwe (hawapo pichani) alipotembelea mkoa huo jana , kushoto ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Bw. Herman Paul Tesha.[/caption]

Na: Zawadi Msalla-WHUSM

Watumishi wa Mkoa wa Songwe wameshauriwa kuwa na utamduni wa kufanya kazi kwa  bidii ikiwa ni nyenzo muhimu ya kufikia malengo na azma iliyowekwa na Serikali ya Awamu ya Tano ya kuifanya Tanzania kuwa  nchi  ya Viwanda.

Hayo yamezungumza na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo  Prof. Elisante Ole Gabriel wakati alipokutana na Sekretarieti ya Mkoa huo,na kuwaeleza  kuwa ni wakati muafaka kwa watumishi kupata  na kutoa elimu sahihi ya kuwafanya wananchi wapende utamaduni wa kufanya kazi kwa bidii bila kulazimishwa.

[caption id="attachment_5395" align="aligncenter" width="750"] Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole akiangalia moja ya kazi za filamu iliyoandaliwa na wasanii wa Mkoa wa Songwe alipotembelea mkoa huo jana, kushoto ni Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo Bw. Herman Paul Tesha[/caption]

“Ni vizuri watumishi wakawa na elimu ya kutosha kuhusu utamaduni wa kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia maadili ya kiutumishi ili kuweza kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kufanya kazi kwa maendeleo ya nchi yetu,” alisema Prof. Elisante

Prof. Elisante aliongeza kuwa  ni muhimu  kwa watumishi wa Umma na watanzania kwa ujumla kufanya  kazi  kwa kushirikiana  ili kutekeleza  majukumu yao ya kila siku kwa manufaa ya taifa .

[caption id="attachment_5398" align="aligncenter" width="750"] Wazee wa kimila kutoka koo mbalimbali za Mkoani Songwe walipokutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel (hayupo pichani) jana mkoani hapo.[/caption]

Aidha alieleza kuwa ni budi Watanzania kufuata maadili na kuzingatia muda katika  utunzaji  wa rasilimali za nchi kwa manufaa ya kizazi kilichopo na kijacho kwa kuwa ni vigumu kutegemea mtu kutoka nje ya nchi  kutunza rasilimali za nchi yetu.

Vilevile Prof. Elisante aliwaomba watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa  wa Songwe kuunga mkono jitihada za Rais John Pombe Magufuli za kuipeleka mbele nchi katika uchumi wa kati na kuwa Taifa la Viwanda.

[caption id="attachment_5401" align="aligncenter" width="1000"] Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akisikiliza maelezo ya kimondo kilichopo Mkoani Songwe wakati wa ziara yake Mkoani hapo.(Picha na Zawadi Msalla-WHUSM)[/caption]

Katika hatua nyingine Prof.Elisante aliipongeza Wilaya ya Ileje kwa kuwa mfano katika utendaji uliopelekea  mafanikio makubwa kwa mkoa wa Songwe na kuzitaka Wilaya nyingine kuiga mfano huo.

Naye Kaimu Katibu Tawala Mkoa huo Bw.Herman Tesha aliahidi kutekeleza ushauri ulitolewa na Katibu Mkuu Prof.Elisante licha ya uchanga wa mkoa wake kwa kuwa  anaamini mwamko na ari ya watumishi waliopo kwa pamoja wanaweza kuleta maendeleo.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi