Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Taarifa kwa Umma
Jan 04, 2019
Na Msemaji Mkuu

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb) amepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Mwanamuziki nguli wa Muziki wa Dansi nchini  Bw. Abdallah Mgonahazeru aliyefariki dunia jana jijini Dar es Salaam.

Hadi anafikwa na umauti, Bw. Mgonahazeru alikuwa Kiongozi wa Bendi ya Vijana Jazz (SAGA RHUMBA). Marehemu pia amewahi kuwa Mwanamuziki katika Bendi za Cuban Marimba pamoja na Madevela Sound.

Waziri Mwakyembe ametoa pole kwa  familia ya marehemu, ndugu, jamaa na   marafiki, Uongozi wa Vijana Jazz, Uongozi  Chama cha Muziki wa Dansi na Shirikisho la Muziki nchini pamoja na wanamuziki wote kwa kuondokewa na mpendwa wao.

Imetolewa na

Anitha Jonas

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,

Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.

04/01/2019

 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi