Rais Dkt. Mwinyi Ahudhuria Maziko ya Askofu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Zanzibar
Sep 16, 2022
Na
Jacquiline Mrisho
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akihudhuria maziko ya Marehemu Askofu Mstafu wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Zanzibar, John Ramadhan yaliyofanyika katika Kanisa la Mkunazini leo tarehe 17-9-2022 na (kulia kwa Rais) ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Ikulu, Mhe. George Mkuchika na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Khamis Ramadhan Shaban
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akitoa heshima za mwisho kwa mwili wa Marehemu Askofu Mstafu wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Zanzibar leo tarehe 17-9-2022. Maziko yaliyofanyika katika viwanja vya Kanisa la Anglikana Mkunazini Wilaya ya Mjini Unguja.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyiakiweka mchanga katika kaburi la Marehemu Askofu Mstafu wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Zanzibar, John Ramadhan, maziko hayo yamefanyika katika viwanja vya Kanisa la Mkunazini Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar leo tarehe 17-9-2022.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyiakiagana na Viongozi wa Kanisa la Anglikana Mkunazini Zanzibar baada ya kumalizika kwa maziko ya Askofu Mstafu Marehemu John Ramadhan yaliyofanyika leo tarehe 17-9- 2022 katika viwanja vya Kanisa la Mkunazini Wilaya ya Mjini Unguja Jijini Zanzibar.