Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Ofisi ya Waziri Mkuu Yafanya Kikao na Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar
Oct 13, 2022
Na Jacquiline Mrisho

Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu imepata ugeni kutoka Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar ambao umelenga katika kubadilishana uzoefu katika masuala ya kazi, maendeleo vijana, ukuzaji ajira na ustawi wa Watu wenye Ulemavu.

Ugeni huo umeongozwa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais anayesimamia masuala ya Kazi, Uchumi na Uwekezaji. Katika kikao hicho, ofisi hizo zimedhamiria kushirikiana kwa karibu katika kutekeleza majukumu sambamba na kutoa huduma kwa wananchi kwa tija na ufanisi katika pande zote mbili za Muungano.

Aidha, katika kikao kazi hicho, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – Kazi, Uchumi na Uwekezaji aliambatana na Kamishna wa Kazi – Zanzibar pamoja na Mkurugenzi wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSH) – Zanzibar.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi