Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mpina Afufua Kiwanda cha Nyama Shinganya
Apr 10, 2018
Na Msemaji Mkuu

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina (Mwenye Miwani) akioneshwa eneo la kiwanda cha nyama Shinyanga na Mkurugenzi wa Ubinafsishaji na Ufuatiliaji kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina Jones Mwalemba (aliyenyoosha mkono) kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Uzalishaji Mifugo na Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Asimwe Lovince kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Wilaya a shinyanga wa CCM.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ametoa siku saba kwa wawekezaji wa kiwanda cha nyama Shinyanga cha Kampuni ya Triple S Beef Limited na Agri Vision kuwasilisha hati zote za umiliki hati ya eneo la kiwanda na eneo la kuhifadhia mifugo baadha ya kushindwa kukiendeleza kwa miaka 11.

Akizungumza katika kiwanda hicho leo Mpina amuagiza Mkurugenzi wa Ubinafsishaji na Ufuatiliaji Jones Mwalemba kutoka Hazina kuhakikisha kwamba ifikapo Juni 30 mwaka huu kiwanda hicho kiwe kimempata mwekezaji ambaye ataanza kazi mara moja ya uchinjaji ili kutoa ajira na kuliingizia taifa mapato.
Aidha amemuagiza Msajili wa Hazina kuanza uhakiki wa mali zote za kiwanda hicho baada ya kubainika wizi uliokithiri katika kiwanda hicho.Pia Mpina ameamuru mmliki wa Kampuni inayolinda kiwanda hicho kukamatwa mara moja na kufikishwa katika mikono ya sheria kwa ajili ya kujibu mashitaka wa wizi wa mali za kiwanda hicho ambapo amemtaka Mkuu wa Mkoa kuhakikisha kuanzia sasa kiwanda hicho kilindwe na vyombo vya Serikali badala ya makampuni binafsi.
Waziri Mpina alisema hatua ya Kampuni ya Triple S kuuza kiwanda na kuingia mkataba mpya na Kampuni ya Agrovisioni ni kinyume na mkataba wa awali ilioingia na Serikali.“Huu ni ukiukwaji wa masharti ya Mkataba kulingana na kifungo cha 16.1 ambapo sasa kinauondoa umiliki wake katika kiwanda hiki” alisisitiza MpinaMkurugenzi wa Uzalishaji na Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Lovince Asimwe kiwanda kilianza ujenzi wake mwaka 1975 na kwamba kimegharimu dola za kimarekani milioni tatu na kilijengwa na Serikali kwa ufadhili wa Benki ya Dunia. Alisema mwaka 2007 kiwanda hicho kilibinafsishwa kwa mwekezaji Tripple S Beef Limited lakini kutoka na na matatizo ya uendeshaji kiwanda hicho kilifungwa mwaka 2017 na kukabidhiwa kwa Serikali.

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi