Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Blogu ya Idara ya Habari - MAELEZO

Mkandarasi Soko la Kariakoo Atakiwa Kuongeza Kasi
Oct 31, 2023
Mkandarasi Soko la Kariakoo Atakiwa Kuongeza Kasi
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais -TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatius Mativila (aliyeinama) akikagua moja ya vizimba jana alipokagua mradi wa ujenzi na ukarabati wa soko la Kariakoo uliofikia asilimia 91.
Na Mwandishi Wetu

Mkandarasi anayejenga na kukarabati soko la Kariakoo Estim Construction Limited  ametakiwa kuongeza kasi ya kukamilisha mradi huo ili  taratibu za kuwarejesha wafanyabiashara zikamilishwe.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu ,Ofisi ya Rais-TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatius Mativila mara baada ya kutembelea na kukagua utekelezaji wa mradi huo uliofikia asilimia 91 jijini Dar es Salaam jana (Oktoba 30,2023).

"Mradi wa ukarabati na ujenzi wa soko la Kariakoo hadi sasa umefikia asilimia 91 na utakamilika hivi karibuni ambapo tunategemea zaidi ya wafanyabiashara 3,500 wapate nafasi za kufanya biashara katika mazingira ya kisasa, hivyo serikali inataka kuona Mkandarasi akiongeza kasi ili mradi huu uwezeshe shughuli za kiuchumi kuendelea sokoni," alisema Mhandisi Mativila.
 

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais - TAMISEMI anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatius Mativila (shati la bluu mbele) akikagua moja ya miudombinu ya soko la kuu la Kariakoo linalokarabatiwa jana jana Dar es Salaam.



Mhandisi Mativila alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha shilingi bilioni 28.3 zilizofanikisha mradi huo ikiwa ni lengo la kuwajali wananchi wapate eneo bora na la kisasa la kufanyia biashara.

Kaimu Meneja Mkuu Shirika la Masoko ya Kariakoo, Bw. Sigsbert Valentine akizungumza na Waandishi wa Habari jana Dar es Salaam kuwa taratibu za kuwarejesha wafanyabiashara zinaendelea kukamilishwa na kuwa zitakuwa za uwazi.
 



Kwa upande wake Kaimu Meneja Mkuu wa Shirika la Masoko ya Kariakoo, Sigsibert Valentine alisema maandalizi ya taratibu za kuwerejesha wafanyabiashara sokoni  yanaendelea na utakuwa ni wa uwazi.

Mradi huo unatekelezwa kufuatia janga la moto lililotokea Julai 10, 2021 ambapo serikali imetoa shilingi bilioni 28.03 ili kufanikisha ujenzi na ukarabati ulioanza Januari 2022 na ulitarajiwa kukamilika Oktoba mwaka huu kupitia mkandarasi Estim  Construction Limited ya Dar es Salaam na mtaalam mshauri akiwa ni Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).


 

Mipangilio
Marekebisho ya Mandhari
Marekebisho ya Maandishi